Na Ahmed Mahmoud,Killimanjaro.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Annaclair Shija amewasimamisha watumishi wawili wa hospitali ya wilaya hiyo akiwemo  Afisa Tabibu kwa kudai na kupokea rushwa ya shs. 15,000/= kutoka kwa mama mwenye mtoto mchanga  mgonjwa wakike mwenye umri wa miezi mitano wa kijiji cha Vunta kilichopo ukanda wa milimani mwa wilaya hiyo.

 Shija amechukua hatua hiyo baada ya afisa tabibu huyo Kimweri kihiyo amesimamishwa kwa kumwandikia upasuaji mtoto huyo ambao hakustahili na kudai rushwa hiyo huku mlinzi daniel kihara  alimuuzia dawa kutoka bohari ya serikali kwashs. 4,500/ kwa mama wa mtoto huyo ambaye alistahili apewe mtoto wa miaka 12.

 Aidha amesema,  vitendo vya aina hiyo vimekuwa vikiidhalilisha serikaliambayo imekuwa ikitoa fedha nyingi kwa ajili ya dawa ambazo zinapatikana kwa asilimia 90 na kitendo cha kumwandikia dawa na upasuaji ambao hakustahili ni sawa mauaji .

Muuguzi wa hospitali hiyo bw  Fabian Bulili  amesema kuwa afisa tabibu huyo ambaye hakuwa kazini anaonyesha alikuwa na tabia ya kuwaandikia dawa wagonjwa kwa ushirikiano na watumishi wasio waaminifu na kujipatia fedha kuikosesha mapato halmashauri

Baadhi ya wananchi wa wilaya hiyo  eliabu mgonja wameipongeza hatua hiyo na kueleza kuwa watumishi wa aina hiyo wanastahili kufukuzwa kazi ili wananchi waendelee kupata huduma bora za afya bila kudaiwa rushwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...