Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
MREMBO kutoka Afrika Kusini Zozibini Tunzi (26) amejinyakulia taji la Miss Universe kwa mwaka 2019 akizibwaga nchi 87 zilizoshiriki mashindano yaliyofanyika huko Atlanta nchini Marekani.
Zozibini amevalishwa taji hilo usiku ya jumapili ya Desemba 08 baada ya kupitia katika raundi zote huku akijibu vyema maswali yaliyohusu jamii ikiwemo ni kueleza kwanini awe chaguo katika mashindano hayo
Moja ya maswali ambayo Zozibini alijibu baada ya kuulizwa kwanini awe chaguo la kuwa Miss Universe alisema kuwa;
"Nimekua katika dunia ambayo mwanamke kama mimi mwenye ngozi na nywele za aina yangu haijawahi kuzingatiwa kuwa ni mwanamke mzuri, ninafikiri ni wakati wa kuacha hili leo, ninataka watoto wangu wanitizame na kuona sura zao zikiakisi yangu" ameeleza mlimbwende huyo.
Washindi waliofuatia ni mrembo kutoka Mexico (Miss Mexico) na mrembo kutoka Puerto Rico.
Sophia Aragon ambaye ni Miss Mexico ameeleza kuwa urembo unaweza kutumika kwa namna mbalimbali ambazo zinalenga kusaidia jamii.
Mshindi wa mashindano hayo kwa mwaka 2018 Catriona Gray kutoka Ufilipino ameeleza kuwa mabadiliko yameendelea kufanyika katika mashindano hayo na yana mwelekeo mzuri.
Katika madhindano hayo ambayo yanafanyika kwa mara 68 sasa Tanzania iliwakilishwa na Shubila Shanton Kaigarula (23).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...