*Aelezea hatua kwa hatua namna Watanzania wanavyoshiriki kuleta maendeleo ya nchi yetu
*Ahimiza umuhimu wa kuendelea kulinda amani, umoja, upendo na mshikamano
Na Said Mwishehe-Michuzi Globu ya jamii-Mwanza
RAIS Dk.John Magufuli amewaongoza maelfu ya Watanzania katika kusherehekea sherehe za miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika ambazo zimefanyika katika Jiji la Mwanza ambapo pia viongozi karibu wote wa Serikali na vyama vikuu vya siasa wamehudhuria.
Wingi wa watu katika sherehe hizo umesababisha baadhi ya wananchi kwenda kukaangalia sherehe hizo katika Uwanja wa Furahisha baada ya uwanja wa CCM Kirumba kujaa na kukosekana nafasi kabisa ya watu kukaa.
Rais Magufuli wakati anazungumza na Watanzania walioko uwanja wa CCM Kirumba leo jijini Mwanza ameelezea furaha aliyonayo katika kusherehekea miaka 58 ya Uhuru wetu ambapo kuna hatua kubwa ya maendeleo ambayo imefanyika kwa nyakati tofauti kuanzia awamu ya kwanza hadi sasa Awamu ya Tano ambayo nayo inaendeleza pale ambapo watangulizi wengine wameishia.
Hata hivyo amesema kuwa sababu za kufanyika Mwanza kwa sherehe hizo ni kuondoa mazoea ambayo yameoeeleka kuwa kuna mikoa fulani ndiko ambako zifanyikie. Pia amesema kuwa ifahamike sherehe za Uhuru hazikufanyika kwa miaka miwili, mwaka 2015 na mwaka 2018.
"Fedha ambazo zilitengwa kwa ajili ya sherehe katika miaka hiyo zilikwenda kutumika kufaya maendeleo ya Watanzania.Tunafahamu sherehe hizo huambatana na fursa mbalimbali, kuchochea maendeleo ya mkoa huo na leo hii pamoja na mambo mengine tunajivunia amani iliyopo nchini kwetu tangu tumepata uhuru, tumeendeelea kulinda umoja na mshikamano.
"Hii ni siku muhimu kwa Watanzania wote lakini nikiri Mwanza mmefunika , mmejitokeza kwa wingi sana katika sherehe hizi ukingalisha na maeneo mengine.Hongereni sana, nimeambiwa uwanja umejaa, kule nje kumejaa, Uwanja wa Furahisha umejaa, hii haijawahi kutokea. Siku kama ya leo Desemba 9, mwaka 1961 Tanganyika ilipata Uhuru wake kutoka kwa wakoloni,"amesema Rais Magufuli.
Ameongeza kuwa uhuru huo ulitokana na jitihada za Watanganyika wakiongozwa na Baba wa Taifa Mwalim Julius Nyerere ambaye alikuwa mstari wa mbele na shupavu katika kusimamia misingi ya kuwaunganisha Watanganyika na hatimaye kupata uhuru.
Ametumia nafasi hiyo kutoa pongezi kwa wazee wetu 17 ambao Julai 7 mwaka 1954 walishiriki kikao cha kwanza baada ya TANU ambayo ilifanikisha kupatikana kwa Uhuru wetu. "Hawa wazee wanastahili pongezi kutokana mchango ambao wameutoa kwa Taifa letu."
Pia amewapongeza viongozi waliopita pamoja na Watanzania wote kwa mafanikio ambayo nchi yetu imepata tangu kupata Uhuru wake mwaka 1961.Pamoja na mafanikio amesema kujenga nchi nako kuna changamoto zake, hivyo ni vema wananchi wote wakaendelea kushirikiana kuhakikiha nchi inasonga mbele kimaendeleo.
"Hivyo jukumu la kizazi cha sasa ni kuendeleza pale walipoishia watangulizi. Kinachofurahisha zaidi nchi yetu amani imeendelea kuimarika, nchi yetu imekuwa yenye umoja na mshikamano, namshhukuru Rais Shein (Dk. Ali) ambaye tunashirikiana kulinda Muungano wetu kikamilifu,"amesema.
Ameongeza Uhuru ambao tuliupata mwaka 1961 ni hatua za mwanzo za kujikomboa kisiasa lakini sasa ni wakati wa kuendelea kuweka mipango kwa ajili ya kujikomboa kiuchumi. Kujenga nchi si lelemama, ni kazi ngumu na tumevuka milima na mabonde, hivyo leo hii ni fursa ya kufanya tathmini kuhusu wapi tumefikia, katika ujenzi wa taifa letu.
"Na katika hilo napenda kutumia fursa hii kuzipongeza awamu zote ambazo zimetangulia kwani zimefanya kazi kubwa ya kujenga nchi yetu.
"Kila awamu imefanikiwa kufanisha majukumu yake kuanzia Awamu ya Kwanza iliyoongozwa na Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Awamu ya Pili ya Mzee Mwinyi (Ali Hassan), Awamu ya Tatu Mzee Mkapa (Benjamin) pamoja na Awamu ya Nne ya Mzee Kikwete (Jakaya)".
Ametaja baadhi ya mafanikio ambayo yamepatikana ni kuendelea kudumishwa kwa amani nchini. Amani iliyopo imesababisha nchi kusifika ndani na nje ya Bara la Afrika.
Rais Magufuli amesema kuwa mafanikio mengine ni katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii ambapo ametumia nafasi hiyo kuelezea hatua kwa hatua maendeleo ambayo yamefanyika nchini.
"Nitoe mifano michache wakati tunapata Uhuru baada ya kutawaliwa na wakoloni kwa takribani miaka 76 nchi yetu ilikuwa na barabara za lami zinazounganisha mkoa na mkoa, wilaya na wilaya zilikuwa kilometa 360 tu. Kipande cha barabara ya Dar e s Salaam hadi Morogoro pamoja na kipande cha Tanga-Korogwe na Arusha- Moshi.
"Kwa sasa tuna barabara za lami kilometa 12,679.55, wakati kilometa nyingine zaidi ya 2400 zinaendelea kujengwa kwa kiwangon cha lami huku pia kilometa 7,087 zipo kwenye hatua mbalimbali za maandalizi kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami,"amesema.
Pia amesema madaraja ambayo yamejengwa nchini madogo ni zaidi ya 8,000, ya kati zaidi ya 79 na madaraja makubwa 17 na mengine yapo kwenye hatua mbalimbali ikiwamo daraja ya Busisi ambalo ujenzi wake umezinduliwa kwa kuwekwa jiwe la msingi na daraja la Salender jijini Dar es Salaam.
Katika huduma za afya, Rais Magufuli amesema kwa nchi ilipokuwa inapata uhuru kulikuwa na vituo vya kutolea huduma za afya 1,095, yaani hospitali 98, vituo vya afya 22 na zahanati 975, lakini sasa idadi imeongezeka kwa kiwango kikubwa. "Kuna vituo vya afya 7,293, hospitali 178, na zahabati 6,285."
Kuhusu shule alisema mwaka 1961 kulikuwa na shule za msingi 3,100 na sasaa kuna shule za msingi 17,379, wakati shule za sekondari zilikuwa 41, leo hii kuna sekondari 4,817, Chuo Kikuu, kilikuwa kimoja na sasa kuna vyuo vikuu 48.
Amesema hiyo ni mifano michache kati ya mingi kutokana na maendeleo ambayo yamefanyika nchini kwetu ambapo alitumia nafasi hiyo kuelezea kuongeza kwa watumishi wa umma wa kada mbalimbali ikiwemo kada ya madaktari waliosajiliwa ukilinganisha na huko nyuma.
*Ahimiza umuhimu wa kuendelea kulinda amani, umoja, upendo na mshikamano
Na Said Mwishehe-Michuzi Globu ya jamii-Mwanza
RAIS Dk.John Magufuli amewaongoza maelfu ya Watanzania katika kusherehekea sherehe za miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika ambazo zimefanyika katika Jiji la Mwanza ambapo pia viongozi karibu wote wa Serikali na vyama vikuu vya siasa wamehudhuria.
Wingi wa watu katika sherehe hizo umesababisha baadhi ya wananchi kwenda kukaangalia sherehe hizo katika Uwanja wa Furahisha baada ya uwanja wa CCM Kirumba kujaa na kukosekana nafasi kabisa ya watu kukaa.
Rais Magufuli wakati anazungumza na Watanzania walioko uwanja wa CCM Kirumba leo jijini Mwanza ameelezea furaha aliyonayo katika kusherehekea miaka 58 ya Uhuru wetu ambapo kuna hatua kubwa ya maendeleo ambayo imefanyika kwa nyakati tofauti kuanzia awamu ya kwanza hadi sasa Awamu ya Tano ambayo nayo inaendeleza pale ambapo watangulizi wengine wameishia.
Hata hivyo amesema kuwa sababu za kufanyika Mwanza kwa sherehe hizo ni kuondoa mazoea ambayo yameoeeleka kuwa kuna mikoa fulani ndiko ambako zifanyikie. Pia amesema kuwa ifahamike sherehe za Uhuru hazikufanyika kwa miaka miwili, mwaka 2015 na mwaka 2018.
"Fedha ambazo zilitengwa kwa ajili ya sherehe katika miaka hiyo zilikwenda kutumika kufaya maendeleo ya Watanzania.Tunafahamu sherehe hizo huambatana na fursa mbalimbali, kuchochea maendeleo ya mkoa huo na leo hii pamoja na mambo mengine tunajivunia amani iliyopo nchini kwetu tangu tumepata uhuru, tumeendeelea kulinda umoja na mshikamano.
"Hii ni siku muhimu kwa Watanzania wote lakini nikiri Mwanza mmefunika , mmejitokeza kwa wingi sana katika sherehe hizi ukingalisha na maeneo mengine.Hongereni sana, nimeambiwa uwanja umejaa, kule nje kumejaa, Uwanja wa Furahisha umejaa, hii haijawahi kutokea. Siku kama ya leo Desemba 9, mwaka 1961 Tanganyika ilipata Uhuru wake kutoka kwa wakoloni,"amesema Rais Magufuli.
Ameongeza kuwa uhuru huo ulitokana na jitihada za Watanganyika wakiongozwa na Baba wa Taifa Mwalim Julius Nyerere ambaye alikuwa mstari wa mbele na shupavu katika kusimamia misingi ya kuwaunganisha Watanganyika na hatimaye kupata uhuru.
Ametumia nafasi hiyo kutoa pongezi kwa wazee wetu 17 ambao Julai 7 mwaka 1954 walishiriki kikao cha kwanza baada ya TANU ambayo ilifanikisha kupatikana kwa Uhuru wetu. "Hawa wazee wanastahili pongezi kutokana mchango ambao wameutoa kwa Taifa letu."
Pia amewapongeza viongozi waliopita pamoja na Watanzania wote kwa mafanikio ambayo nchi yetu imepata tangu kupata Uhuru wake mwaka 1961.Pamoja na mafanikio amesema kujenga nchi nako kuna changamoto zake, hivyo ni vema wananchi wote wakaendelea kushirikiana kuhakikiha nchi inasonga mbele kimaendeleo.
"Hivyo jukumu la kizazi cha sasa ni kuendeleza pale walipoishia watangulizi. Kinachofurahisha zaidi nchi yetu amani imeendelea kuimarika, nchi yetu imekuwa yenye umoja na mshikamano, namshhukuru Rais Shein (Dk. Ali) ambaye tunashirikiana kulinda Muungano wetu kikamilifu,"amesema.
Ameongeza Uhuru ambao tuliupata mwaka 1961 ni hatua za mwanzo za kujikomboa kisiasa lakini sasa ni wakati wa kuendelea kuweka mipango kwa ajili ya kujikomboa kiuchumi. Kujenga nchi si lelemama, ni kazi ngumu na tumevuka milima na mabonde, hivyo leo hii ni fursa ya kufanya tathmini kuhusu wapi tumefikia, katika ujenzi wa taifa letu.
"Na katika hilo napenda kutumia fursa hii kuzipongeza awamu zote ambazo zimetangulia kwani zimefanya kazi kubwa ya kujenga nchi yetu.
"Kila awamu imefanikiwa kufanisha majukumu yake kuanzia Awamu ya Kwanza iliyoongozwa na Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Awamu ya Pili ya Mzee Mwinyi (Ali Hassan), Awamu ya Tatu Mzee Mkapa (Benjamin) pamoja na Awamu ya Nne ya Mzee Kikwete (Jakaya)".
Ametaja baadhi ya mafanikio ambayo yamepatikana ni kuendelea kudumishwa kwa amani nchini. Amani iliyopo imesababisha nchi kusifika ndani na nje ya Bara la Afrika.
Rais Magufuli amesema kuwa mafanikio mengine ni katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii ambapo ametumia nafasi hiyo kuelezea hatua kwa hatua maendeleo ambayo yamefanyika nchini.
"Nitoe mifano michache wakati tunapata Uhuru baada ya kutawaliwa na wakoloni kwa takribani miaka 76 nchi yetu ilikuwa na barabara za lami zinazounganisha mkoa na mkoa, wilaya na wilaya zilikuwa kilometa 360 tu. Kipande cha barabara ya Dar e s Salaam hadi Morogoro pamoja na kipande cha Tanga-Korogwe na Arusha- Moshi.
"Kwa sasa tuna barabara za lami kilometa 12,679.55, wakati kilometa nyingine zaidi ya 2400 zinaendelea kujengwa kwa kiwangon cha lami huku pia kilometa 7,087 zipo kwenye hatua mbalimbali za maandalizi kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami,"amesema.
Pia amesema madaraja ambayo yamejengwa nchini madogo ni zaidi ya 8,000, ya kati zaidi ya 79 na madaraja makubwa 17 na mengine yapo kwenye hatua mbalimbali ikiwamo daraja ya Busisi ambalo ujenzi wake umezinduliwa kwa kuwekwa jiwe la msingi na daraja la Salender jijini Dar es Salaam.
Katika huduma za afya, Rais Magufuli amesema kwa nchi ilipokuwa inapata uhuru kulikuwa na vituo vya kutolea huduma za afya 1,095, yaani hospitali 98, vituo vya afya 22 na zahanati 975, lakini sasa idadi imeongezeka kwa kiwango kikubwa. "Kuna vituo vya afya 7,293, hospitali 178, na zahabati 6,285."
Kuhusu shule alisema mwaka 1961 kulikuwa na shule za msingi 3,100 na sasaa kuna shule za msingi 17,379, wakati shule za sekondari zilikuwa 41, leo hii kuna sekondari 4,817, Chuo Kikuu, kilikuwa kimoja na sasa kuna vyuo vikuu 48.
Amesema hiyo ni mifano michache kati ya mingi kutokana na maendeleo ambayo yamefanyika nchini kwetu ambapo alitumia nafasi hiyo kuelezea kuongeza kwa watumishi wa umma wa kada mbalimbali ikiwemo kada ya madaktari waliosajiliwa ukilinganisha na huko nyuma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi katika sherehe za miaka 58 ya Uhuru wa Tanzania Bara pamoja na miaka 57 ya Jamhuri zilizofanyika katika uwanja wa CCM Kirumba jijjini Mwanza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...