Mvua hizo zilizosababisha kifo cha mkazi mmoja pia zilipelekea nyumba nyingi kuwa chini ya maji kwa muda wa siku ya Jumamosi Novemba 30 mwaka huu. 

Baada ya kufanya ziara hiyo ambapo aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara, imebainika kuwa mafuriko hayo katika maeneo hayo yamechangiwa na ujenzi holela juu ya njia asili za maji ambapo pia imebainika kwamba ujenzi huo umefanywa kwa ridhaa ya baadhi ya watu katika nafasi za Mamlaka husika.

Mkuu wa Mkoa.ameagiza kwamba Viongozi wa Manispaa ya Musoma chini ya usimamizi wa Mkuu wa wilaya wafanye tathmini mara moja kubaini uzembe huo uliofanyika na wahusika na hatua stahili zichukuliwe.

Aidha.ametumia nafasi hiyo kuongea na wananchi na kuwasihi kuchukua tahadhari na taratibu za usalama wa maeneo yao. Amewakumbusha kutumia nafasi hiyo kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba maji hayo yalifurika saa za mchana na watu walipata nafasi ya kujiokoa, kwani kama maji hayo yangevamia maeneo hayo usiku wananchi wakiwa wamelala maafa yangekuwa makubwa sana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...