Urusi imefungiwa kwa miaka minne kushiriki michezo yoyote mikubwa ya kimataifa na wakala wa kupambana na dawa za kusisimua misuli (Wada).

Inamaanisha kuwa bendera ya Urusi haitapepea wala wimbo wao wa taifa wa nchi yao hautapigwa kwenye michuano kama ya Olimpiki ya mwaka 2020 na michuano ya kandanda ya kombe la dunia ya mwaka 2022 nchini Qatar.

Lakini kwa wanamichezo ambao watathibitisha kutotumia dawa hizi wataruhusiwa kushiriki lakini kwa kigezo cha kutoiwakilisha Urusi.

Kamati kuu ya Wada imefanya maamuzi haya katika mkutano wake mjini Lausanne, Switzerland.

Hatua hii inakuja baada ya wakala wa kupambana na dawa za kusisimua misuli nchini Urusi (Rusada) kutajwa kutotii na kuziharibu sampuli za wanamichezo wa Urusi Januari 2019.

Hata hivyo ilitakiwa kusiwasilisha sampuli hizo kwa Wada baada ya tuhuma zilizopelekea kufungiwa kwa miaka mitatu kuanzia mwaka 2018.

Wada inasema Rusada ina siku 21 kukata rufaa. Kama haitofanya hivyo pendekezo hilo litafikishwa katika mahakama kuu ya michezo (Cas).

Makamu Rais wa Wada Linda Helleland amesema zuio hili ''halitoshi''

''Binafsi nilitaka kuwepo vikwazo ambavyo vitakua vikali zaidi,'' alisema.''Tunapaswa kuwasafisha wanamichezo ambao hawahusiki na vikwazo hivi kwa kadri tuwezavyo''
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...