Rwanda imezindua kampeni yake ya kwanza ya kutoa chanjo dhidi ya virusi vya Ebola. Zaidi ya watu elfu mbili na mia mbili wamekufa kutokana na ugonjwa huo katika nchi jirani ya Jamuhuri ya kidemokrasi ya Congo tangu mwezi Agosti mwaka jana.
Waziri wa afya wa Rwanda, Diane Gashumba, alisema watu laki mbili wanatarajiwa kupata chanjo hiyo katika maeneo yanayopakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kipaumbele kitapewa wafanyikazi wa afya, maafisa wa uhamiaji, polisi na wale wanaojihusisha na biashara ya mipakani.
Ni kwa nini Rwanda iliamua kutoa chanjo hiyo ilhali haijakabiliwa na ugonjwa wa Ebola?
Kampeni ya kutoa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Ebola ilizinduliwa jana katika mji wa Rubavu kaskazini magharibi mwa Rwanda , mji unaopakana na mji wa Goma nchini DRC. kampeni hii itakuwa ikiendelea hata katika mji wa Rusizi kusini magharibi mwa Rwanda,mji unaopakana na mji wa Bukavu pia nchini Congo.
Rwanda haijakabiliwa na ugonjwa wa Ebola,lakini miji yake ya Rubavu na Rusizi inafanya biashara kubwa na nchi ya Congo,na ni miji yenye uingiliano mkubwa wa wananchi kutoka nchini mbili.
Waziri wa afya wa Rwanda, Diane Gashumba, alisema watu laki mbili wanatarajiwa kupata chanjo hiyo katika maeneo yanayopakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kipaumbele kitapewa wafanyikazi wa afya, maafisa wa uhamiaji, polisi na wale wanaojihusisha na biashara ya mipakani.
Ni kwa nini Rwanda iliamua kutoa chanjo hiyo ilhali haijakabiliwa na ugonjwa wa Ebola?
Kampeni ya kutoa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Ebola ilizinduliwa jana katika mji wa Rubavu kaskazini magharibi mwa Rwanda , mji unaopakana na mji wa Goma nchini DRC. kampeni hii itakuwa ikiendelea hata katika mji wa Rusizi kusini magharibi mwa Rwanda,mji unaopakana na mji wa Bukavu pia nchini Congo.
Rwanda haijakabiliwa na ugonjwa wa Ebola,lakini miji yake ya Rubavu na Rusizi inafanya biashara kubwa na nchi ya Congo,na ni miji yenye uingiliano mkubwa wa wananchi kutoka nchini mbili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...