Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
WAKIWA na jumla ya miaka 211 John (106) na Charlotte  Henderson (105)Desemba 15 wataadhimisha miaka 80 ya ndoa yao huku wakieleza siri ya mafanikio yao ni kutengeneza kesho bora zaidi kuliko leo.

Kwa mujibu wa mtandao wa Guinness World Record imeelezwa kuwa wanandoa hao waishio Texas nchini Marekani walikutana mwaka 1934 katika Chuo cha Texas ambapo Charlotte alikiwa akisomea masuala ya elimu na John alikuwa mcheza mpira maarufu chuoni hapo.

Licha ya kutobahatika kupata mtoto wawili hao wameeleza kuwa siku zote wamekuwa wakishirikiana katika masuala mbalimbali  Kama vile kucheza pamoja na kufanya mazoezi.

Charlotte amemwelezea mumewe John kuwa ni mwelewa sana na mwenye moyo wa kusamehe;

"Hatukumbushiani mambo yaliyopita baada ya kusamehe, tunaishi kwa furaha na mapenzi ya hali ya juu" ameeleza.

Kwa upande wake John amemwelezea mkewe kuwa ni mwanamke anayejali na wamekuwa wakizidi wakifurahia kila siku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...