RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Katibu wa
Kamati ya Uhamasishaji na Halaiki Zanzibar. Ndg. Ali Mohammed
Bakari(Shasha) alipowasili katika viwanja vya Polisi Ziwani Zanzibar
kuhudhuria hafla ya Chakula Maalum alichowaandalia Vijana wa Halaiki
katika sherehe za Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar
zilizofanyika katika Uwanja wa Amaan 12,January 2020.(Picha na Ikulu).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa amesimama na
Viongozi wa meza kuu wakati ukipigwa wimbo wa Taifa, (kulia kwa Rais)
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.Mhe. Balozi Seif Ali Iddi na Katika
Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Abdulhamid Yahya
Mzee na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar
Mhe. Riziki Pembe Juma.(Picha na Ikulu)
BAADHI ya Veteran wa Young Pioneer
walioshiriki katika Gwaride la Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya
Zanzibar, wakiwa wamesimama wakati ukipigwa wimbo wa Taifa, kabla ya
kuaza kwa hafla ya Chakula Maalum kilichoandaliwa na Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, kwa Vijana
wa Halaiki walioshiriki sherehe za Maadhimisho ya Miaka 56 ya
Mapinduzi ya Zanzibar, zilizofanyika Uwanja wa Amaan 12,January 2020,
hafla hiyo imefanyika katika Viwanja vya Polisi Ziwani Zanzibar.(Picha
na Ikulu)
BAADHI ya Vijana walioshiki
katika Halaiki ya Madhimisha ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar,
zilizofanyika katika Uwanja wa Amaan Zanzibar,12,January , wakiwa
wamesimama wakati ukipigwa wimbo wa Taifa baada ya kuwasili Mgeni rasmin
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali
Mohamed Shein.(hayupo pichani) katika hafla ya Chakula Maalum
alichowaandalia Vijana hao katika viwanja vya Polisi Ziwani
Zanzibar.(Picha na Ikulu).
KATIBU wa Kamati ya Uhamasishaji
na Halaiki Zanzibar .Ndg. Ali Mohammed Bakari (Shasha) akizungumza na
kutowa shukrani kwa niaba ya Washiriki wa Halaiki ya Maadhimisho ya
Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar, zilizofanyika katika Uwanja wa Amaan
Zanzibar 12,January.2020, wakati wa hafla ya Chakula Maalum
kilichoandaliwa kwa ajili ya Vijana hao katika viwanja vya Polisi
Ziwani Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
VIJANA walioshiriki Sherehe za
Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar, zilizofanyika katika
Uwanja wa Amaan Zanzibar,12.January.2020, wakipata chakula Maalum
kilichoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein.(hayupo pichani) katika viwanja vya Polisi
Ziwani Zanzibar.(Picha na Ikulu)
WAZIRI wa Nchi
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Issa Haji Gavu
akizungumza kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, wakati wa hafla ya Chakula Maalum
kilichoandaliwa kwa Vijana walioshiriki Maashimisho ya Miaka 56 ya
Mapinduzi ya Zanzibar , iliofanyika katika Viwanja vya Polisi Ziwani
Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein, akiagana na Makamu wa Pili
wa Rais wa Zanzibar Mhe.Balozi Seif Ali Iddi, baada ya kumalizika kwa
hafla ya chakula maalum kilichoandaliwa kwa ajili ya Vijana walioshiriki
sherehe za Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar, hafla hiyo
imefanyika katika viwanja vya Polisi Ziwani Jijini Zanzibar.(Picha na
Ikulu)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...