Ahmed Mahmoud Arusha.

Imeelezwa kuwa elimu ya  sheria za soka ikitolewa kwa wadau wa mpira ikiwemo mashabiki zitaondoa mkanganyiko na kuwaweka huru marefarii wanaochezesha mpira wa miguu nchini kwa kuwa wadau hao watakuwa na uelewa wa sheria hizo.

Kauli hiyo imetolewa na Makamu mwenyekiti wa shirikisho la soka mkoani Arusha Soud Abdi kwenye kikao cha wadau wa Michezo hususani vyama vya michezo na Waziri wa habari Sanaa Utamaduni na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe kwenye ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha.

Alisema kuwa sheria za soka zinabadilika kila uchwao na wengi wa wadau hawajui sheria hivyo timu zinazoshiriki ligi ziwe zinafundishwa sheria hizo ili kuwawezesha wachezaji kutofanya makosa ambayo yanaweza kuepukika na kuondoa mining'ono ambayo mwisho wa siku lawama nyingi huwaangukia marefarii.

Alimuomba Mh.waziri kukaa na shirikisho la soka kuona namna nzuri ya kuandaa kipindi cha elimu ya sheria za mpira wa miguu kwenye runinga ya taifa kwa kuwa wadau wakijua sheria hizo kutaondoa malalamiko na marefarii watapata ahuweni pia vyama vya soka navyo vitaondokana na dhama ya upendeleo wa timu fulani kutoka kwa timu zinazoshiriki ligi husika.

"Elimu ya sheria ndio jawabu la kuondoa mikanganyiko kwenye mchezo wetu pendwa wa mpira wa miguu kwa hii imewafanya wachezaji wetu kukosa timu ulaya kwa kutojua sheria za mpira tuanze kutoa elimu hii kwenye ligi zetu kuanzia ngazi zote kwa timu shiriki ili kuondokana na ombwe la malalamiko" alisisitiza Abdi

Kwa upande wake waziri Dkt.Mwakyembe aliahidi kukaa na shirikisho la mpira nchini TFF kuona ni jinsi gani sheria zitafundishwa kwenye soka na pia kuahidi wadau hao wa Michezo mkoani Arusha kuanzisha kipindi cha sheria za soka kwenye runinga ya taifa huku akisifu kipindi cha kipenga kwa kupata umaarufu na kuwafanya wadau kujua sheria.

Alisema kuwa sheria za mpira wa miguu zinakuwa na mabadiliko tofauti na zamani hivyo Kuna umuhimu kwa wadau kusijua sheria hizo ili kuendana na mabadiliko hayo sanjari na kutoa elimu hiyo kwa wachezaji wetu kuache kucheza kimazoea.

"Nimekuwa kwenye msongo wa mawazo Sana kwa kuwa wengi wetu mmekuwa mkiandaa timu kizimamoto kushiriki Michezo nje ya nchi jambo hili sio sahihi Sana anzeni mchakato mapema andikeni maandiko mapema na leteni Ofisini kwangu acheni kuendesha Michezo bila maandiko serikali ya Dkt.Magufuli inapenda uwazi kwa kuwa naye napenda Sana Sanaa"alisema Mwekymbe.

Aliwashukuru wanamichezo hususani vyama kwa kuwa wakweli na kutoa maoni yao ili kuboresha Michezo hususani mashuleni na kuahidi kukaa na wizara ya elimu kuona mtaala wa Michezo unafanyiwa kazi kwa kuwa Michezo ni ajira kubwa Sana kwenye dunia ya Sasa.

"Hapo awali tulifuta Michezo mashuleni tujikite kuzalisha wahandisi,madaktari lakini bila Michezo yote ni kazi bure ndio maana tukarudisha Michezo mashuleni yaende sambamba na masomo mengine kwa lengo la kuongeza akili za wanafunzi  hivyo ntakaa na wenzangu kuona tunaandaaje shule moja kwa kila mkoa badala ya kuwa na utitiri wa shule za Michezo"

Suala la kuwa na wataalamu wenye uzoefu na Michezo hususani kwenye chuo cha Michezo Malya alisema amegundua jambo hivyo Sasa kuona umuhimu wake ili kuboresha taaluma ya Michezo kwa kuwa na wakufunzi wenye taaluma za Michezo kusaidia kulipeleka taifa kuwa washindani kwenye Michezo kwa siku za usoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...