Na Khadija seif, Michuzi Tv
KWENYE
tano bora ya wasanii wanaopeperusha bendera ya Tanzania kwenye Muziki
wa bongofleva huwezi kumuacha kumtaja msanii Rajab Harmonize.
Harmonize
alipokua akifanya mahojiano na kituo cha redio nchini amesema kwa mwaka
huu anatarajia kufanya show yake katika ukumbi wa 02 arena uliopo
nchini uingereza huku akiweka wazi kuwa malipo tayari yameshafanyika
yeye kufanya show hiyo juni mwaka huu.
"Natumaini
nitaweka historia ya kuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika mashariki
kufanya show katika ukumbi huo mkubwa wa burudani,"
Aidha,
harmonize amefafanua kuwa alipokua uwanja wa vila pack kwenye mechi ya
leister city dhidi ya Aston Villa alishuhudia shangwe na vifijo pale
mchezaji kutoka nchini Tanzania Mbwana Samata alipoingia uwanjani kwa
mara ya kwanza mara baada ya kusajiliwa na klabu ya aston Villa.
"Juzi
nilivokua uwanjani nilithibitisha hilo kwani ndio mara yake ya kwanza
kuingia dimbani kupitia timu ya Aston Villa tangu asajiliwe lakini bado
mashabiki walikua wakipiga yowe na wakitaja jina lake wakiwa na imani
nae jambo kama hilo linatia sana hamasa sana kwake na kitaifa pia kuona
hatuangushi hasa kwenye sekta ya michezo na kuipeperusha bendera ya
Tanzania,"



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...