Na.Khadija seif, Michuzi Tv

WABUNIFU washauriwa kutengeneza mavazi yanayoendana na mazingira halisi ili kuweza kupata vitu vya kiasili na kutangaza utalii zaidi.

Akizungumza na Michuzi Tv mbunifu mkongwe Ally Remtullah ambae siku chache amefungua duka lake la mavazi akishirikiana na Kampuni ya high_ flyge ambao walisaini mkataba wa  kuuza nguo za aina ya kitenge ya nchini  china.

"Wabunifu wengi wamekua wakitengeneza nguo ambazo zinatumia malighafi za nchi za wenzetu lakini kwa upande wangu nimeamua kujikita kwenye vitenge na kanga kwani hazibagui mtu jinsia watu wote hupendeza,"

Hata hivyo Remtullah ameeleza kuwa yupo tayari kusupport wabunifu chipukizi na kuwatafutia masoko nje na ndani ya nchi.

"Nawakaribisha wabunifu chipukizi kuleta bidhaa zao kwenye duka langu lililopo Msasani barabara ya chole,"

Pia ametoa shukrani za dhati kwa wadau na viongozi wanaoendelea kumpa moyo na hata wale wanaounga mkono sekta ya ubunifu wa mavazi hasa vazi la kitenge huku akifafanua kuwa anawaheshimu na kupenda kazi za wabunifu wengine Kama Martin kadinda, Khadija mwanamboka pamoja na Mustafa hassanali.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...