Na Woinde Shizza,Arusha

 Imeelezwa kuwa Mkoa wa Arusha unakabiliwa na upungufu wa madawati
elfu 25000 pamoja na vyumba vya madarasa  elfu moja .

Hayo yamebainishwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo wakati
alipokuwa akipokea msaada wa madawati 18  yaliyotolewa na benki ya
Frist National Bank (FNB) kwa ajili ya kupunguza tatizo hilo katika
shule zilizopo mkoani hapa

Gambo alibainisha kuwa japo kuwa kunaupungufu wa madawati hayo pamojacna vyumba vya madarasa lakini hakuna mwanafunzi hata mmoja ambaye ameacha kwenda shule kutokana na tatizo hilo .

“tunaupungufu wa madawati kweli na madarasa  katika wilaya zetu za
mkoa wa Aursha lakini sisi kama mkoa tumehakikisha hakuna mwanafunzi
hata mmoja ambaye ameacha kuja shule au anakaa chini  kutokana na
tatizo hilo ,wanafunzi wote wapo shule lakini kitu ambacho kinatokea
ni kwamba kama dawati lilitakiwa kukaa watoto wawili sisi tumeongeza
wanakaa watatu haya yote ni kuhakikisha watoto wetu wanaingia darasani
kupata elimu  kama inavyotakiwa huku tukiangalia namna ya kutatua
tatizo hili”Alibainisha Gambo

Alisema kuwa anashukuru sana kwa benki hii kuwapatia msaada huu huku
akichukuwa nafasi hiyo kuwataka  wakuu wote wa wilaya za Arusha
kutobweteka kutokana na kuona baadhi ya wadau wanaleta msaada wa
madawati badala yake wafanye kazi kwa bidii ili kuhakikisha tatizo
hili linamalizika haraka sana kwa mkoa wa Arusha .

Kwa upande wake katibu tawala wa mkoa wa Arusha Richard Kwitega
alisema kuwa msaada huu wamadawati utawasaida kwa kiasi kikubwa
kuimarisha na kuboresha  elumu kwani  ,miundo mbinu ya elimu ikiwa
vizuri  taaluma itapanda na watoto wataweza kufaulu vizuri

Alisema mkoa wa Arusha  unampango  wa  kuanza kufanya mitiani ya
miuhal ili kuimarisha elimu na kuongeza ufaulu zaidi  ,hivyo aliwata
wadau hawa kuendele akushirikiana  ili waweze kuleta maendeleo ya
kitaaluma katika mkoa huu ,huku akisisitiza kuwa jukumu la maendeleo
katika huu  ni lakila mdau

 Kwa upande wake katibu tawala wa wilaya ya Arusha D avid John
Mwakiposa aliwashukuru  benki hii kwakutoa msaada huu ambapo alisema
utawasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo hilo ,huku akiwataka
wadau mbalimbali,sekta binafsi,pamoja na tasisi kujitokeza kusaidia
kumaliza tatizo hili.

Naye  meneja wa Benki ya  FNB  tawi la Arusha Edna Kalape alisema kuwa
 wameamua kujitolea kusaidia tatizo hili na watajitaidi kusaidia zaidi
pale ambapo wataweza ili kumaliza kabisa changamoto hizi.
  Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa amempa
mkono meneja wa tawi la benki ya  First national Bank(FNB)  mkoa wa
Arusha  Edna Kalape isha ya kupokea msaada wa madawati kwa ajili ya
shule za mkoa wa Arusha juzi(jana) ambapo benki hiyo imetoa madawati
18 kwa ajili ya shule za mkoa wa Arusha ambapo kwa mujibu wa mkuu wa
mkoa huo amesema kuwa hadi sasa mkoa wa huo unaupungufu wa madawati elfu 25000(picha na Woinde Shizza ,Arusha ).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...