Na Woinde
Shizza, Michuzi TV Arusha
Walimu wa shule
binafsi nchini wamelalamikia kutokushirikishwa katika usimamizi wa mitihani ya
kitaifa pamoja na usahihishaji licha ya kuwa nguzo muhimu katika
maendeleo ya elimu nchini na kuchangia katika kukuza ubora wa elimu.
Akizungumza katika
Mkutano wa Chama cha Walimu wa Shule binafsi nchini ,Katibu Mkuu wa Chama
hicho Julius Mabula mkutano uliofanyika juzi(jana ) katika ukumbi wa golden
rose jijini Arusha ameiomba serikali iwashirikishe katika kusimamia na
kusahihisha mitihani ya kitaifa kwani kwa miaka mingi wamekua hawashirikishi
licha ya kuwa na sifa stahiki kama walimu wa shule za serikali
“sisi tunasifa kama
vile walimu wengine wa shule za serikali wanazo lakini kinachotushangaza
atushirikishwi katika swala lolote la usahihishaji mitiani wala usimamizi wa hii mitiani kwa ufupi naweza sema
tumetegwa sisi walimu wa shule binafsi “Julius
Mabula
Alisema kuwa
watafurahi sana kuona kwamba serikali inatambua uwepo wa kwa kuwashirikisha
katika mambo mbalimbali ya uhusuyo elimu
kwani nguzo muhimu katika maendeleo ya ellimu ni kushirikiana na kuchangia kukuza ubora wa
elimu
Kwa upande wake mgeni
rasmi wa mkutano huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega
alisema kuwa serikali imepokea maombi ya walimu wa shule binafsi katika
kusimamia mitihani ya kitaifa na watayafikisha kwenye ngazi husika ili yaweze
kufanyiwa kazi
“tumesikia maombi yenu
na tumeyapokea na napenda kuwahaidi kuwa tutafikiksha maombi haya katika ngazi
husika ili yaweze kufanyiwa kazi hivyo niwaambie usiwe na hofu kwani serikali
yenu ni sikivu na itafanyia kazi haya “alibainisha Richard Kwitega
Kwa upande wake Rais
wa chama wa walimu wa shule binafsi nchini Cornel Bukolo hicho pamoja na wadau wa elimu
wamesema kuwa walimu wa shule binafsi wanapaswa kushirikishwa katika mipango ya
kuboresha elimu na kupatiwa mafunzo ili kukuza kiwango cha elimu na kufikia
nchi yenye uchumi wa kati .
Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega akiongea katika mkutano huo


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...