Wajukuu wa Malkia nchini Uingereza William na Harry wameipuuza ripoti ya gazeti moja hii leo inayozungumzia kuwepo mvutano mkubwa katika uhusiano wao, wakisema taarifa hiyo ni ya kukera na ya uharibifu mkubwa wakati wakirejea kwenye mazungumzo kuhusiana na mustakabali wa ufalme huo wa Uingereza. 

Ndugu hao wawili walitowa taarifa isiyokuwa ya kawaida hata wakati Malkia Elizabeth wa Pili anapojiandaa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na mwanamfalme Harry kwa mara ya kwanza tangu alipotangaza pamoja na mkewe Meghan mpango wao wenye utata wa kutaka kuyaachia majukumu ya taasisi hiyo ya kifalme. Mkutano huo wa aina yake wa kifamilia unalenga kuweka mwelekeo wa mustakabali wa wanandoa hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...