Wajukuu wa Malkia nchini Uingereza William na Harry wameipuuza ripoti
ya gazeti moja hii leo inayozungumzia kuwepo mvutano mkubwa katika
uhusiano wao, wakisema taarifa hiyo ni ya kukera na ya uharibifu mkubwa
wakati wakirejea kwenye mazungumzo kuhusiana na mustakabali wa ufalme
huo wa Uingereza.
Ndugu hao wawili walitowa taarifa isiyokuwa ya kawaida hata wakati Malkia Elizabeth wa Pili anapojiandaa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na mwanamfalme Harry kwa mara ya kwanza tangu alipotangaza pamoja na mkewe Meghan mpango wao wenye utata wa kutaka kuyaachia majukumu ya taasisi hiyo ya kifalme. Mkutano huo wa aina yake wa kifamilia unalenga kuweka mwelekeo wa mustakabali wa wanandoa hao.
Ndugu hao wawili walitowa taarifa isiyokuwa ya kawaida hata wakati Malkia Elizabeth wa Pili anapojiandaa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na mwanamfalme Harry kwa mara ya kwanza tangu alipotangaza pamoja na mkewe Meghan mpango wao wenye utata wa kutaka kuyaachia majukumu ya taasisi hiyo ya kifalme. Mkutano huo wa aina yake wa kifamilia unalenga kuweka mwelekeo wa mustakabali wa wanandoa hao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...