WAZIRI wa madini Dotto Biteko amewataka wafanyakazi wa shirika la madini nchini (STAMI O) kuendelea kushirikiana na wanachama nchi nzima hasa kwa kuwasikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili.

Akizungumza katika mkutano huo wa baraza la wafanyakazi Waziri Biteko amesema kuwa shirika hilo limepiga hatua kubwa sana hasa kwa kutoka kwenye hatua ya kuzalisha madeni ya shilingi bilioni 63 bila faida na hadi kufikia sasa hakuna hakuna deni lolote linalozalishwa.

Amesema kuwa waendeleze miradi itakayowaletea faida ikiwemo mradi wa uchorongaji ulitoa faida ya Shilingi milioni 600 na kumwelekeza Mkurugenzi mkuu kuwachukulia hatua wale wote walioonesha ubadhilifu katika mradi huo.

Vilevile amewataka wafanyakazi wa shirika hilo kufanya kazi kwa ushirikiano pamoja na kutambua mchango wa kila mmoja.

Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa shirika la madini CPA Dkt. Venance Mwese  amesema kuwa wamepiga hatua kubwa hasa katika masoko ya madini na shughuli za u uchorongaji kwa kandarasi nne kwa shilingi bilioni 2.2 na faida ya shilingi milioni 600.

Ameeleza kuwa wamejipanga  kuboresha shirika hilo ili kuweza kufikia malengo ikiwa ni pamoja na kuongeza mapato kwa serikali na kuinua maisha ya wafanyakazi na mazingira ya ufanyaji kazi.

Aidha amesema kuwa shirika hilo limekuwa na mlengo wa kuacha utegemezi kutoka kwa Serikali ambapo katika bajeti ya mwaka huu asilimia 77 ya bajeti hiyo ya shilingi bilioni 24.5 yametokana na vyanzo vya ndani.
Waziri wa Madini Doto Biteko akizungumza akizungumza na uongozi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) wakati wa kufunga mkutano wa baraza la wafanyakazi wa shirika hilo uliofanyika katika ofisi zao Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Madini, Profesa Simon Msanjila akisisitiza jambo wakati wa kufunga  mkutano wa baraza la wafanyakazi cwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kilichofanyika katika ofisi za Shirika hilo jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Dkt. Venance Mwasse akitoa ufafanuzi kuhusu mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa Shirika hilo kwa Waziri wa Madini Doto Biteko alipofika kufunga mkutano uliofanyika katika ofisi zao zilizopo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) wakimsikiliza Waziri wa Madini Doto Biteko wakati wa kufunga mkutano wa baraza uliofanyika katika ukumbi wa Shirika hilo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Madini Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja  na wafanyakazi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...