Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mh. Altho Komba akizungumza katika kikao cha  Baraza la madiwani la Bajeti lililofanyika katika Ukumbi wa Kepten John Komba Mbamba-bay wilayani hapa,kushoto na Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Nyasa Bw Bernad Semwaiko
……………………………………………………………………………………….
Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa  Mkoani Ruvuma limepitisha Mpango na Bajeti ya TSh.bilioni 24.5 kwa ajili kutekeleza shughuli mbalimbali za Halmashauri zilizopangwa kufanyika kwa mwaka  wa fedha wa 2020/2021.
Mpango huo umewasilishwa na Kaimu Afisa mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Bw. Regius Sanane  katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Kepten John Komba , Mjini Mbamba-bay Wilayani hapa.
Bw. Sanane  alivitaja vyanzo vya mapato hayo kuwa ni makusanyo ya mapato ya ndani, Matumizi mengineyo, Mishahara(PE) na Miradi ya Maendeleo.
Aliongeza kuwa , bajeti hii inalenga ya kujenga msingi imara na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda, kuharakisha maendeleo endelevu,  kuboresha hali ya maisha na ustawi wa jamii, na kuharakisha ustawi wa jamii utakaopunguza umaskini haraka. 
Aidha,aliyataja malengo mengine  ni Kuinua ari ya utendaji kazi wenye tija na ufanisi,kuweka na kuimarisha ushiriki wa wadau wa ndani katika kupanga na kutekeleza mipango mbalimbali na kutmia uwepo wa mazingira mazuri ya nchi yetu kuimarisha shughuli za biashara kwa lengo la kuifanya Taifa letu kuwa Mhimili wa uzalishaji na kitovu cha biashara.
Maeneo mengine ambayo bajeti imezingatia ni ujenzi wa miundombinu ya Elimu ya Msingi na Sekondari, kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya, pamoja na kuongeza uzalishaji mazao ya biashara likiwemo,zao la kahawa,korosho na kokoa. 
Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Altho komba   ametoa wito kwa wataalam  kuendelea na mchakato wa kuiwasilisha bajeti hii sehemu zinazohusika  kwa kuwa Baraza la madiwani limeshapitisha ,na Bajeti hii inalenga kutatua Kero za Wananchi wa Wilaya ya Nyasa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...