Rais Donald Trump ameondolewa mashtaka yaliyokuwa yanamkabili na kumaliza mchakato wa kumuondoa madarakani mchakato ambao uliigawanya vikali Marekani.

Baraza la Seneti, lililoongozwa na Wa-Republican wenzake Rais Trump , lilipiga kura ya kumtoa kwa kura 52-48 kuhustu mashtaka ya matumizi mabaya ya madaraka na kura 53- 47 kuhusu mashtaka ya kuzuia Bunge kufanya kazi yake.
Democrats walimshtaki Bwana Trump mnamo mwezi Desemba na kushinikiza Ukraine kumtia mbaroni mpinzani wa White House.
Mnamo Novemba, Bwana Trump atakuwa rais wa kwanza aliyechukizwa kwenda kwa uchaguzi.
Katika kura yake ya kihistoria Jumatano, Seneti iliamua kutomuondoa rais wa 45 wa Marekani madarakani kwa mashtaka yanayotokana na kushughulika kwake na Ukraine.
Angekutwa na hatia kwa kosa lolote kati ya hayo, Bw. Trump angelazimika kuachia madaraka yake kwa Makamu wa rais Mike Pence.
Ikiwa atapatikana na hatia kwa mashtaka haya yote, Bw Trump angelazimika kuhama ofisi yake na Makamu wa Rais Mike Pence.
Baraza la Wawakilishi linaloongozwa na Kidemokrasia liliidhinisha nakala za mashtaka mnamo tarehe 18 Disemba.
Mashtaka dhidi yaTrump : Kila kitu unachohitaji kujua kuhusu kesi hii
Hii ni mara ya tatu katika historia, ambapo rais wa Marekani anakabiliwa na kesi ya kutumia madaraka vibaya kwa maslahi yake binafsi.
Mashitaka ambayo yanaweza kumpelekea rais Donald Trump kuondolewa madarakani.
Leo ni siku ya pili tangu bunge la seneta wameanza kusikiliza kesi ya rais Trump.
Matokeo yake yanaweza kuleta mshuko mkubwa na tutaeleza sababu zake , lakini kwanza ni vvyema kuelewa maswali ambayo yamekuwa yakiulizwa na watu wengi.
1) Mashitaka dhidi ya rais ni yapi?
Mashitaka haya huwa yanatokana na matumizi mabaya ya madaraka kwa kiongozi kama Jaji, rais na wabunge, kutumia wadhifa wake kwa ajili ya manufaa yake binafsi.
Makosa haya yanajumuisha rushwa,ufisadi,uhaini na uhalifu mwingine.
Baada ya kiongozi kushtakiwa, kesi yake huwa inapelekwa kwenye bunge la seneta na wawakilishi wa baraza huwa wanaamua kama ana hatia au la.Huwa ni kesi ambayo inatatuliwa kisiasa na sio kihalifu.
2) Trump anashutumiwa kwa kosa gani?
Trump anakabiliwa na mashtaka mawili.
Kwanza, anashutumiwa kwa kuomba msaada kwa serikali ya Ukraine kumsaidia achaguliwe tena mwezi Novemba.
Anashutumiwa kwa kusitisha kutoa misaada ya mamilioni ya fedha pamoja na msaada wa kijeshi kwa Ukraine mpaka rais wa nchi hiyo afanye uchunguzi dhidi mpinzani wake.
Uchunguzi wa uhalifu unaomuhusisha Trump na Urusi waanza
Trump ameshutumu "manabii wa kutabiri mabaya" kama Greta Thunberg
Pili , Ikulu ya Marekani kutoruhusu wafanyakazi wake wote kutoa ushaidi dhidi ya Trump wakati kesi ya rais huyo iliposikilizwa wa mara ya kwanza mwaka jana.
Bwana Trump alikanusha kuhusika na makosa yote na kikosi chake cha sheria na kudai kuwa madai haya ni hatari sana na huo ni upotoshaji wa katiba.
Ilikuwa sawa kuwa madai haya hayana uhusiano na uchunguzi wa Urusi kuingilia uchaguzi wa Mwaka 2016.
3) Kwa nini kulikuwa na kesi?
Hatua kadhaa zilipita ili madai haya kuitwa kesi:
Agosti 2019: Watu walitoa madai dhidi ya rais Trump
Oktoba - Disemba: Uchunguzi ulifanyika , licha ya chama cha Trump kuwa na viti vingi zaidi ya wapinzani wake.
Disemba:Kiongozi wa Democratic alipiga kura kumshtaki rais Trump
Januari 2020: Kesi ilifikishwa kwa seneti


Wajumbe Seneti Wamehitimisha Kesi Ya Matumizi Mabaya Ya Madaraka na Kulizuia Bunge Kutekeleza Majukumu dhidi Rais Donald Trump kwa kupiga kura ya Kumuondolea Mashtaka hayo.
Shtaka la Kwanza: Matumizi Mabaya ya Madaraka.
Matokeo ya kura:
(1) Republican -52
(2) Democrat - 48
Shtaka la Pili: Kuzuia Bunge Kutekeleza Majukumu Yake.
(1) Republican - 53
(2) Demokrat - 47
Matokeo ya Kura Yanasomwa na Jaji Mkuu Robert. Matokeo Hayo yanamaanisha Rais Trump ataendelea kusalia Madarakani baada ya kufutiwa mashtaka yote mawili yaliyokuwa yanamkabili.
=====

Chanzo: BBC Swahili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...