Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT),Dkt Bernard Kibesse (wa pili kushoto), na Mwenyekiti wa Bodi wa Benki ya Absa Tanzania, Simon Mponji (kulia), wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Benki ya Absa Tanzania ambayo awali ikiitwa Barclays Benki Tanzania. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Emmanuel Kakwezi, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed na Mkurugenzi wa Chama cha wenye Mabenki (TBA), Tuse Jumbe.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Absa Tanzania, Simon Mponji, akipokea cheti cha kubadilisha jina la kufanyia biashara kama Benki ya Absa Tanzania kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Emmanuel Kakwezi (wa pili kushoto), katika hafla ya uzinduzi rasmi wa benki ya Absa Tanzania jijini Dar es Salaam jana. Awali iliitwa Benki ya Barclays Tanzania. Wanaoshuhudia kutoka ni; Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed na Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, (BoT), Bernard Kibesse (wa pili kulia) pamoja na washuhudiaji wengine.
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT),Dkt Bernard Kibesse akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Benki ya Absa Tanzania ambayo awali ikiitwa Barclays Benki Tanzania. Wengine kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi wa Benki ya Absa Tanzania, Simon Mponji, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed, Mkuu wa Kitengo cha Sheria na udhibiti wa Benki hiyo, Irene Sengati.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Benki ya Absa Tanzania ambayo awali ikiitwa Barclays Bank Tanzania.
Wafanyakazi wa Benki ya Absa Tanzania wakifanya maandamano ya amani kuashiria uzinduzi rasmi wa Benki ya Absa Tanzania ambayo awali ikiitwa Barclays Benki Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...