Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua kadi ya
bima ya afya ngazi ya jamii iliyoboreshwa kutoka kwa mgonjwa aliyefika
hospitali ya Wilaya ya Mwanga kupata huduma za afya.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto)
akionyesha alama ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika
dawa zote ambazo zinatolewa Serikali kwa Mbunge wa Jimbo la Mwanga Prof.
Jummane Maghembe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto)
akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bw. Thomas Apson (kulia) mara
baada ya kuwasili katika ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Mwanga.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua uwekaji
wa kumbukumbu za taarifa za jotoridi la jokofu la dawa katika Hospitali
ya Wilaya ya Mwanga.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia)
akifafanua jambo kwa watumishi wa Wilaya ya Mwanga (hawapo pichani)
kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bw. Thomas Apson.
Mbunge wa Jimbo la Mwanga Prof.
Jumanne Maghembe akisema jambo kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani)
wakati wa Ziara ya Dkt. Ndugulile Wilayani Mwanga.
………………………………………………………………………………………………………….
Na WAMJW – Mwanga, Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameutaka uongozi
wa Hospitali ya Wilaya ya Mwanga kuandaa mkakati madhubuti
utakaowawezesha kuwa na vipimo muhimu vya afya.
Dkt Ndugulile ametoa agizo hilo
leo alipotembelea Hospitali ya Wilaya ya Mwanga kujionea hali ya utoaji
huduma na kubaini kuwa hospitali hiyo haina vipimo vya damu, vipimo vya
kemia pamoja vipimo vya CD4.
”Kwa miaka miwili sasa hakuna vipimo vya msingi katika hospitali hii, tunawakosesha huduma wananchi” amesema Dkt. Ndugulile
”Haiwezekani Hospitali kubwa ndani
ya Wilaya kukosa vipimo vya msingi, haiwezekani mtu hapa sasa hivi
anahitaji kipimo cha damu atoke hapa aende Hospitali ya Mawenzi Moshi
kwa ajili ya vipimo” amesema Naibu Waziri Ndugulile.
Katika hatua za kutafuta ufumbuzi
wa changamoto hiyo, Waziri Ndugulile ameushauri uongozi wa afya ndani ya
Wilaya kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga kuhakikisha wanatenga
fedha kwa ajili ya kununua vifaatiba hivyo ili wananchi waweze kupata
huduma za vipimo ndani ya Wilaya ya Mwanga.
Aliendelea kushauri kuwa kupitia
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wao wanatoa mkopo wa majengo na
vifaa kwa taasisi za umma na binafsi, mnaweza kuwafikia NHIF na kujadili
kuhusu suala hili.
”Huko kwingine wanazitumia hizo
fursa, kaeni na watu wa NHIF, Meneja wa NHIF kaa na viongozi wa
Hospitali hii ikiwezekana mkubaliane hivyo vitu vipatikane kwa haraka”
ameshauri Dkt. Ndugulile.
”Naamini mna wadau wa maendeleo
ambao mnashirikiana nao katika mambo mbalimbali, timu ya afya ndani ya
mkoa, wilaya pamoja na hospitali nawaombeni sana tuwe tunaomba vitu
ambavyo vina manufaa kwa wananchi” amesisitiza Dkt. Ndugulile.
Awali akitoa salamu za wananchi wa
Wilaya ya Mwanga, Mbunge wa Jimbo la Mwanga Profesa Jumanne Maghembe
amesema kuwa changamoto ya kijiografia ndani ya Wilaya hiyo inachangia
wananchi kukimbilia hospitali za Wilaya jirani ili kuweza kupata huduma.
”Wilaya yetu hii ina upande wa
mlimani na huku tambarare, wananchi wengi walio huku tambarare wanaona
ni bora kwenda Moshi kwa ajili ya matibabu kuliko kwenda juu mlimani
iliko Hospitali” amesema Prof. Maghembe.
Hata hivyo Prof. Maghembe amesema
kuwa tayari ndani ya Wilaya wameshaanza taratibu za kujenga Hospitali
nyingine eneo la chini (tambarare) ili wananchi wanaoishi maeneo hayo
waweze kupata huduma za afya ndani ya Wilaya ya Mwanga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...