Charles James, Michuzi TV
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma linamshikilia mwanaharakati huru Cyprian Musiba kwa kutuhuma za kusambaza habari za kutaka kuuliwa bila kuripoti kwenye vyombo vya dola jambo ambalo ni kinyume na Sheria.
Akizungumza na Wandishi wa Habari leo Feb.24.2020 jijini Dodoma Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto amesema Musiba kupitia baadhi ya magazeti hapa nchini amechapisha kulalamika kutishiwa kuuwawa na baadhi ya wanasiasa .
" Tunamshikilia kwa mahojiano ili aweze kutueleza kwa undani juu ya malalamiko hayo anayoyatoa, na hii ni kwa sababu yeye mwenyewe licha ya kulalamika kutaka kuuliwa hajatoa ripoti zozote kwa Jeshi letu," Amesema Muroto.
Hivyo Kamanda Muroto ametoa Rai kwa wananchi kuacha tabia ya kutoa habari za makosa ya jinai kwenye vyombo vya habari bila kujulisha vyombo vya dola na jeshi hilo linamshikilia Musiba kwa Mahojiano zaidi dhidi ya Malalamiko yake.
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma linamshikilia mwanaharakati huru Cyprian Musiba kwa kutuhuma za kusambaza habari za kutaka kuuliwa bila kuripoti kwenye vyombo vya dola jambo ambalo ni kinyume na Sheria.
Akizungumza na Wandishi wa Habari leo Feb.24.2020 jijini Dodoma Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto amesema Musiba kupitia baadhi ya magazeti hapa nchini amechapisha kulalamika kutishiwa kuuwawa na baadhi ya wanasiasa .
" Tunamshikilia kwa mahojiano ili aweze kutueleza kwa undani juu ya malalamiko hayo anayoyatoa, na hii ni kwa sababu yeye mwenyewe licha ya kulalamika kutaka kuuliwa hajatoa ripoti zozote kwa Jeshi letu," Amesema Muroto.
Hivyo Kamanda Muroto ametoa Rai kwa wananchi kuacha tabia ya kutoa habari za makosa ya jinai kwenye vyombo vya habari bila kujulisha vyombo vya dola na jeshi hilo linamshikilia Musiba kwa Mahojiano zaidi dhidi ya Malalamiko yake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake jijini Dodoma leo kuhusiana na kumshikilia mwanaharakati huru, Cyprian Musiba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...