Katika kuunga
mkono jitihada za Serikali za kupambana na uharibifu wa mazingira unaosababisha
athari kubwa za Mabadiliko ya Tabia Nchi, Chuo Kikuu Mzumbe kimeanza kampeni ya
upandaji Miti; ikiwa ni sehemu ya kutekeleza Sera yake ya Mazingira.
Makamu Mkuu wa
Chuo Prof. Lughano Kusiluka ameongoza mamia ya wanafunzi kutoka Kitivo cha
Sayansi na Teknolojia (FST) kupanda miti zaidi ya 1000 kwenye eneo la Barabara
kuu kuingia Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi Kuu eneo la Maekano Kata ya Mzumbe Wilaya
ya Mvomero.
Akizungumza mara baada ya kushiriki zoezi
hilo; Makamu Mkuu wa Chuo alishukuru ushirikiano mkubwa wa wanafunzi kushiriki
zoezi hilo; na kwamba kitendo hicho kitabaki kuwa historia katika Maisha yao
kwakuwa watakuwa wameacha alama isiyofutika.
“Ushiriki wenu
umeacha kumbukumbu ya kesho kwakuwa hata mtakapomaliza shule mtakumbuka miti
ambayo mmeipanda na kuancha alama. Huu ni moyo wa kizalendo na ambao mnapashwa
kuwarithisha wengine kujali na kulinda mazingira ili kuondokana na athari kubwa
za mabadiliko ya tabia nchi yanayochangiwa kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa
mazingira” Alisema
Aidha ameahidi
Chuo Kikuu Mzumbe kuendelea kuwa mabalozi wema katika kampeni ya upandaji miti,
na kwamba tayari kama chuo wana sera ya Mazingira inayotoa dira ya kutunza
mazingira na kuunga mkono jitihada za Serikali katika kulinda mazingira.
Mkuu wa Kitivo
cha Sayansi na Teknolojia wa Chuo Kikuu Mzumbe Dr. Joseph Sungau amesema
waliamua kuanza na kampeni ya kupanda miti kama sehemu ya elimu kwa wanafunzi
kwa kutambua kazi kubwa ya miti kisayansi katika kupambana na madhara
yatokanayo hewa chafu inayozalishwa na shughuli za kibinadamu vikiwemo viwanda,
magari na mitambo mbalimbali na kwamba kwa kupanda miti kwa kiasi kikubwa kinapunguza
athari za uwepo wa hewa chafu.
“Tumeanza na
miti hii michache lakini lengo letu ni kuendelea kuwafundisha wanafunzi wetu
sayansi kwa vitendo kwa kuanza na masuala haya ya upandaji miti ambayo
yanafaida za moja kwa jamii.
Zoezi hilo
ambalo lilifanyika kwa kushirikisha Chuo Jirani SUA kupitia wakala wa kimataifa
wa mazingira “Earth Day Network” limekuwa chachu kwa jamii inayozunguka Chuo
Kikuu Mzumbe kwa kuona umuhimu wa kuendelea kuhamasisha na kutoa elimu kwa
jamii kuhusu faida za upandaji miti.
Makamu Mkuu wa
Chuo Kikuu Mzumbe Prof. Lughano Kusiluka akishiriki kampeni ya upandaji miti
eneo la Maekani Kata ya Mzumbe, Morogoro.
Mkuu wa Kitivo
cha Sayansi na Teknolojia Dr. Joseph Sungau akipanda mti wakati wa kampeni ya
kupanda miti iliyofanywa na Chuo Kikuu Mzumbe. Akishuhudia pembeni ni Makamu
Mkuu wa Chuo Prof. Lughano Kusiluka, na baadhi ya wanafunzi mwaka wa kwanza wa
Kitivo cha Sayansi na Teknolojia.
Mwakilishi wa wakala
wa kimataifa wa mazingira “Earth Day Network” kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) Bi. Zuhura
Ahmed akiwakilisha jumuiya hiyo kwenye shughuli ya upandaji miti iliyofanyika
Maekani Mzumbe– Morogoro. Jumuiya hiyo
inahusisha wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya mkoani Morogoro.
Makamu Mkuu wa
Chuo Kikuu Mzumbe akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki kwenye shughuli ya
upandaji miti Kampasi Kuu – Morogoro.
Vijana wanachuo
wa Chuo Kikuu Mzumbe walioshiriki zoezi la Upandaji miti Maekani wakiwa kwenye
picha ya pamoja; wakati zoezi hilo likiendelea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...