Mwandishi wetu,Longido

Mamlaka ya usimamizi wanyamapori nchini(TAWA) imetaka Kampuni ya Green Miles iliyoondolewa katika kitalu cha uwindaji cha Lake Natron (East),kuondoa vifaa vyake.

Kampuni hiyo iliondolewa na Serikali tangu, January 22 lakini hadi Jana watendaji wa Kampuni hiyo walikuwa hawajajitokeza  kuondoa vifaa vyao kwenye kambi inayolindwa na Askari wa TAWA,polisi na askari mgambo .

Waziri wa Maliasili na Utalii,Dk Hamis Kigwangalla  Agost 7 mwaka jana alitangaza uamuzi wa Serikali kuiondoa Kampuni hiyo Katika kitalu hicho kutokana na kukiuka taratibu za uwindaji ikiwepo migogoro na vijiji.

Hata hivyo, Kampuni hiyo iliomba kuongeza muda hadi Desemba 16 ili kukabidhi kitalu hicho kutokana na wakati uamuzi unatangazwa walikuwa na wageni.
 Afisa wa kikosi cha kupambana na ujangili(KDU) wa TAWA Emmanuel Pius alisema  wanaitaka Kampuni hiyo kuondoa vifaa kwani ndio maamuzi ya Serikali.

"Tangu tuwaondowe Kwa nguvu hapa hawajafika kuondoa vifaa vyao hivyo tunawatakia kufika"alisema 

Hata hivyo alisema wafanyakazi walikuwa wamekamatwa Kwa kupuuza maagizo ya Serikali kuondoka Katika Kitalu hicho waliachiwa Kwa dhamana.
 Hata hivyo Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Awadhi Abdalah amekuwa akipinga kuhusika na mgogoro na vijiji 23 vinavyozunguka Kitalu hicho amba vyo vimekuwa vikidai malimbikizo ya kodi milioni 329.

Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Gilai Lumbwa zilizopo kambi za mwekezaji huyo, Richard Mollel alisema Kwa muda mrefu wana mahusiano mabaya na mwekezaji ikiwepo migogoro ya kushindwa kuwalipa tuzo za vijiji 23.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...