Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mussa Azzan Zungu hii leo ameungana na kikundi cha Pamoja Youth katika zoezi la Upandaji miti katika Shule ya Sekondari Buguruni-Moto. Takriban miti 100 imependwa katika eneo hilo ikiwemo miti ya matunda na miti ya vivuli.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mussa Azzan Zungu akiongea na Bw. Stanslav Toldy raia wa Uingereza akiwa ni sehemu ya wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika uzalishaji wa magari yenye kutumia nishati ya umeme. Wawekezaji hao wamemtembelea Waziri Zungu katika Ofisi ndogo ya Makamu wa Rais, Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mussa Azzan Zungu akiongea na wawekezaji wa Nishati ya kupikia aina ya gesi kutoka Kampuni ya KOPAGas. Kampuni hiyo imelenga kusambaza nishati ya gesi majumbani kwa gharama nafuu kwa mfumo wa ‘kulipia kadiri ya unavyotumia’ Wawekezaji hao wamemtembelea Waziri Zungu katika Ofisi ndogo ya Makamu wa Rais, Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...