Maofisa Waandikishaji wa mfuko wa afya ya jamii ulioboreshwa (ICHF) Wilaya ya Tandahimba wamepewa mafunzo ya ukusanyaji wa fedha kwa njia ya kielektroniki
Akizungumza kwenye ukumbi wa Halmashauri Mratibu wa ICHF Violeth Mahembe alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia kutokuwepo ucheleweshaji Kama ilivyo awali
Alisema awali Waandikishaji walikuwa wanapeleka kuweka fedha kwenye akaunti hivyo kusababisha ucheleweshaji lakini sass itawarahisishia na fedha inayopatikana kwenda sambamba na kaya alizosajili
"Sasa hivi Ofisa Mwandikishaji wa ICHF hatakwenda kuweka fedha benki Bali fedha zote zitaingizwa kwenye mfumo wa serikali kwa njia ya kielectronik," alisema Mahembe
aidha alisema kuwa mafunzo hayo pia yanawahimiza Waandikishaji kuweza kuhamasisha wananchi kujiunga na ICHF iliyoboreshwa ili kuweza kupata huduma za kiafya kwa unafuu kwa kuwasajili kwa njia ya mtandao ( IMS)
Naye Ofisa Mwandikishaji wa Kijiji Cha Mchangani Kata ya Mkoreha Zainabu Linyono alieleza kuwa mafunzo hayo yamewasaidia na watakwenda kufanya kazi kwa ufanisi zaidi
"Kwakweli njia hii itapunguza ucheleweshaji wa kuweka fedha kwakuwa wengine tunakaa vijijini moja ya sababu zilikuwa zinatufanya kutoingiza kwa wakati ," alisema Linyono.
Akizungumza kwenye ukumbi wa Halmashauri Mratibu wa ICHF Violeth Mahembe alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia kutokuwepo ucheleweshaji Kama ilivyo awali
Alisema awali Waandikishaji walikuwa wanapeleka kuweka fedha kwenye akaunti hivyo kusababisha ucheleweshaji lakini sass itawarahisishia na fedha inayopatikana kwenda sambamba na kaya alizosajili
"Sasa hivi Ofisa Mwandikishaji wa ICHF hatakwenda kuweka fedha benki Bali fedha zote zitaingizwa kwenye mfumo wa serikali kwa njia ya kielectronik," alisema Mahembe
aidha alisema kuwa mafunzo hayo pia yanawahimiza Waandikishaji kuweza kuhamasisha wananchi kujiunga na ICHF iliyoboreshwa ili kuweza kupata huduma za kiafya kwa unafuu kwa kuwasajili kwa njia ya mtandao ( IMS)
Naye Ofisa Mwandikishaji wa Kijiji Cha Mchangani Kata ya Mkoreha Zainabu Linyono alieleza kuwa mafunzo hayo yamewasaidia na watakwenda kufanya kazi kwa ufanisi zaidi
"Kwakweli njia hii itapunguza ucheleweshaji wa kuweka fedha kwakuwa wengine tunakaa vijijini moja ya sababu zilikuwa zinatufanya kutoingiza kwa wakati ," alisema Linyono.
Mratibu wa ICHF Wilaya ya Tandahimba Violeth Mahembe
Maofisa Waandikishaji wa mfuko wa afya ICHF wakisikiliza mafunzo
Washiriki wakisiliza kwa makini
Mwezeshaji Cleophace Maulambo akifafanua Jambo kwa washiriki wa mafunzo ya ICHF
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...