
Mashinji amefika mahakamani hapo kisha akaanza kusalimiana na viongozi mbalimbali wa CHADEMA ambao wapo katika kesi moja ambapo miongoni mwao ni Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na Salum Mwalimu.
Lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida, Mbunge wa Kawe Halima Mdee alikataa kumpatia mkono Mashinji huku akiwa busy na simu yake ya mkono.
Aidha Dkt. Mashinji alionana na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe wakiwa ndani ya chumba cha Mahakama licha ya kuwa hawakupeana mikono na mpaka anaondoka mahakamani hapo hawakuonekana kusalimiana.
Hata hivyo Mahakama imepanga kutoa hukumu dhidi ya vigo hao wa CHADEMA Machi 10, mwaka huu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...