Naibu
Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) akijibu maswali ya wabunge
wakati wa Bunge la kumi na nane Jijini Dodoma tarehe 6 Februari 2020.
Sehemu
ya mawaziri akiwemo Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb), Waziri wa
TAMISEM Mhe Suleima Jaffo na Naibu Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi
Mhandisi Hamad Masauni wakifatilia kipindi cha maswali na majibu akijibu
maswali ya wabunge wakati wa BUnge la kumi na nane Jijini Dodoma tarehe
6 Februari 2020.
Naibu
Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) akijibu maswali ya wabunge
wakati wa Bunge la kumi na nane Jijini Dodoma tarehe 6 Februari 2020.
*******************************
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Serikali inatekeleza Mradi wa Kuendeleza Skimu za Umwagiliaji za Wakulima Wadogo (Small Scale Irrigation Development Project -SSIDP) ikiwa ni pamoja na Skimu ya Umwagiliaji ya Nyida.
Naibu Waziri wa
Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) ameyasema hayo Bungeni tarehe 6 Februari
2020 Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe
Azza Hilaly Hamad aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itachimba bwawa
kwa ajili ya kuboresha Mradi wa Umwagiliaji Nyida?
Mhe Mgumba
amesema muwa katika kutekeleza Mradi huo, Kampuni ya Shekemu
Construction Ltd inafanya kazi ya ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya
kuboresha mfumo wa usambazaji maji mashambani ambapo utekelezaji wa
Mradi huo kulingana na Mkataba umefikia asilimia 68 ya kazi zote za
ujenzi.
Ameongeza kuwa
hadi kufikia mwezi Disemba 2019 jumla ya Tsh. 282, 154,880.68 zimelipwa
kwa Mkandarasi kati ya Tsh 466,594,981.81 zilizotengwa kwa ajili ya
kuendeleza Skimu ya Nyida.
Hata hivyo Mradi
huo kwa sasa umesimama kupisha msimu wa kilimo kwa wakulima na mvua
zinazoendelea kunyesha. Hivyo, Mkandarasi ataendelea na kazi iliyobakia
kulingana na Mkataba mara baada wakulima kuvuna mazao yao na Msimu wa
mvua kumalizika.
Mhe Mgumba
amesema kuwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi na mvua zisizotabirika
pamoja na wakulima kuwa na mwamko mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji wa
kutaka kuongeza uzalishaji, tija kwa kulima misimu miwili kwa mwaka na
kwa kuzingatia kuwa chanzo cha maji cha skimu hiyo ni mto Manonga ambao
ni wa msimu na hivyo Serikali iliona umuhimu wa ujenzi wa Bwawa ili
kuendeleza skimu hiyo.
Aidha, ili
kutekeleza mradi huo, mwaka 2013 Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa
kushirikiana na Halmashauri za Wilaya ya Shinyanga na Nzega zilifanya
Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa awali kwenye eneo linalokusudiwa
kujengwa bwawa la Nyida eneo la Lyamalagwa litalokuwa na uwezo wa
kumwagilia maji mita za ujazo 4,167,825 na gharama ya shilingi 3.5
bilioni kwa wakati huo.
Kadhalika,
Kutokana na mabadiliko ya kimuundo ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, na
miradi mingi ya umwagiliaji kujengwa chini ya kiwango, Serikali
haikuweza kutekeleza mradi huo kwa wakati kutokana kufanya tathmini ya
kina ya ufanisi ya miradi hiyo na hivyo kushindwa kutekeleza mradi kwa
wakati.
Aidha, kwa kuwa
muda mrefu umepita tangu tahtmini hiyo ifanyikke, Serikali itafanya
mapitio upya ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kupata mahitaji
na gharama halisi ya ujenzi wa bwawa na athari zake kwa sasa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...