Na.Khadija seif, Michuzi Tv

MSANII wa singeli Mwarami Sadick maarufu Kama meja kunta alietamba na kibao cha ooh mamuu amepata  ajali alfajiri ya kuamkia leo maeneo ya segera mkoani Tanga.

Akizungumza na Michuzi Tv kupitia simu Meneja wa Meja Waso wiso amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

"Tumepata ajali maeneo ya segera Tanga na kwenye gari tulikua na cameraman,dj ,mimi pamoja na Meja mwenyewe tumegongana na gari ambapo ajali inatokea meja alikua amelala na yeye ndio ameumia sana,"

Hata hivyo waso wiso amesema ilikua ngumu kwao kupata msaada wa haraka kutokana na ilikua asubuhi sana na kumtaja madee pamoja na Naibu waziri wa maji Juma Aweso kuwa msaada kwao.

"Madee alikua ni miongoni mwa wasanii ambao walikua wanaelekea kwenye Tamasha la Muziki mnene hivyo ikawa rahisi kutuona barabarani akisaidiana na Naibu waziri wa maji Juma Aweso na kutupatia msaada wa haraka.

Hata hivyo Waso ameeleza kuwa Hali ya Meja sio nzuri hivyo wamelazimika kumkimbiza hospitali ya mkoa ili kupatiwa matibabu zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...