Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
UINGEREZA
imejiondoa rasmi katika Muungano wa nchi za Ulaya (EU) na kuwa nchi ya
kwanza kujiondoa katika umoja huo ambao umedumu kwa miaka 47 kabla ya
kuamua kujiondoa kupitia mchakato wa kura za maoni .
Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson alitangaza mwanzo mpya kwa Uingereza kabla ya kujiondoa.
Kujiondoa
kwa Uingereza (brexit)ambako kumeelezwa kuwa ni jambo la kihistoria
kumefanyika usiku kwa saa sita kwa saa za Uingereza ambapo maandamano na
shangwe vimeelezwa kukafanyika kwa baadhi ya maeneo ambayo yalipiga
kura ya kuruhusu kujiondoa.
Waziri Boris ameahidi kuleta nchi hiyo pamoja na kulipeleka taifa hilo mbele zaidi.
Baada
ya Uingereza kujiondoa katika umoja huo raia nchini humo watashuhudia
mabadiliko machache yanayoanza moja kwa moja baada ya nchi hiyo
kujiondoa kwenye Muungano wa Ulaya.
Licha
ya sheria nyingi za Ulaya kuendelea kuwepo ikiwa ni pamoja na usafiri
huru wa raia hadi Desemba 31 mwaka huu ambapo kipindi cha mpito
kitakuwa kinafikia ukomo.
Licha
ya kujiondoa katika umoja huo Uingereza inalenga kutia saini
makubaliano ya biashara huru na Umoja wa Ulaya, wenye kufanana na ule wa
Muungano wa Ulaya na Canada.
Wachambuzi
wa mambo kutoka nchi za Ulaya wamenukuliwa wakisema kuwa Uingereza
itapitia wakati mgumu kufikia makubalino ndani ya siku ya ukomo
iliyowekwa.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...