Tanzania imeieleza  Tume ya haki za binadamu na watu wa Afrika ya Umoja wa Afrika kuwa kuna tofauti kati ya makosa ya kitaalamu na makosa ya jinai na kwamba Sheria inapochukua mkondo wake isitafsirike kuwa ni kukiuka haki za binadamu kwa kuwa Nchini Tanzania hakuna raia wake yeyote aliye juu ya sheria pale anapotenda kosa la jinai.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameyasema hayo katika majadiliano ya taarifa ya Tume ya Haki za Binadamu katika mkutano wa 33 wa Baraza la Mawaziri wa Umoja wa Afrika unaofanyika Addis Ababa Nchini Ethiopia na kuongeza kuwa Tanzania inaheshimu haki za binadamu,uhuru wa kujieleza na uhuru wa vyombo vya habari kama ilivyo katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Prof. Kabudi ameongeza kuwa Nchini Tanzania hakuna raia wake aliye juu ya sheria na kwamba pale mwanataaluma anapofanya makosa ya kijinai huchukuliwa hatua za kisheria kama ilivyo kwa wananchi wengine kwa kufikishwa katika vyombo rasmi vya kutoa haki kama mahakama ambayo iko huru kufanya maamuzi yake isichukuliwe kama ukiukwaji wa haki za binadamu au kuminya uhuru wa kujieleza.

Amesema kuwa kuna baadhi ya wananchi wa Tanzania ambao wamekuwa wakitumia taaluma zao vibaya na hivyo kuwafanya kutenda makosa ya jinai kwa kutumia taaluma zao na hivyo kufikishwa mbele ya sheria na kuongeza kuwa mashauri yao yako mahakamani na vyombo vingine vya sheria na ana imani mahakama na vyombo hivyo vitatoa haki dhidi ya mashtaka yanayowakabili baada ya kutoa utetezi wao mbele ya vyombo hivyo.

Hivi karibuni kumekuwepo na mjadala kutoka kwa baadhi ya wanaharakati,wanasiasa na Jumuiya za Kimataifa zikiishutuma Tanzania kukiuka haki za binadamu jambo ambalo serikali imeiambia Umoja wa Afrika na Jumuiya za Kimataifa kuwa si kweli na kwamba Tanzania inaheshimu haki za binadamu na uhuru wa kujieleza.

Mkutano wa kawaida wa 33 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika unafanyika Mjini Addis Ababa Nchini Ethiopia ukitanguliwa na mikutano mbalimbali ya Baraza la Mawaziri na baadae Wakuu wa Nchi na Serikali na unatarajiwa kumalizika Februari 10,2020. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...