*Vibali na Usajili vilihusisha Dawa, Vifaa Tiba na Vitendanshi
*Yapiga hatua katika uanzishaji wa viwanda vya dawa,vifaa tiba Kanda ya Ziwa.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii ,Mwanza
Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Ziwa katika kipindi cha miaka minne ya serikali ya awamu ya tano ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli imesajili na kutoa vibali vya majengo ya biashara ya Dawa, Vifaa Tiba na Vitandanishi 2,043.
Usajili na utoaji wa vibali ilitokana na TMDA Kanda ya ziwa baada ya kufanya ukaguzi na kujiridhisha kuwa majengo yankidhi vigezo vya utunzaji wa ,usambazaji ,uuzaji na utengenezaji wa bidha hizo.
Akizungumza na waandishi wa habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto , Meneja wa Kanda ya Ziwa Sophia Mziray amesema kuwa katika Miaka minne ya Utawala wa Rais Dkt.John Pombe Magufuli wamefanikiwa kutokana na serikali kuwekeza maabara ya uchunguzi wa dawa,Vifaa Tiba na Vitendanishi kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa za afya zilizo bora.
Amesema kuwa TMDA kwa kanda Ziwa imetoa ushauri wa kitaalamu katika kiwanda cha dawa kimoja cha jijini Mwanza pamoja na ushauri wa wa kiufundi kwa kwa viwanda saba vipya vya tiba na viwanda vinne vya vipya vya dawa za maji na sindano.
Mziray amesesma TMDA imeweka wakaguzi katika mipaka vituo vya forodha vya Sirari, Mtukula na Bandari ya Mwanza Kusini ambao ndio wakaguzi wa dawa,vifaa tiba na vitendanishi kuruhusu kuingia au kutoka nje ya nchi mara tu baada ya kujiridhisha katika ukaguzi.
Aidha amesema kuwa wameanzisha mfumo wa Kieletroniki wa uombaji wa vibali na utoaji kwa masaa 24 ambapo kupitia mfumo huu mkaguzi aliyeko mpakani ay bandarini anaweza kuhakikisha kibali kilichotolewa na mamlaka wakati wa kufanya ukaguzi wa bidhaa inayoingia kutoka nje ya nchi hadi sasa jumla ya vibali 2552 vimetolewa.
“Kwa kazi inayofanyika inaonyesha kuwa elimu ya udhibiti kwa wadau wetu imeeleweka na hivyo kukidhi matakwa ya kisheria ya uingizaji na utoaji wa bidhaa nje ya nchi”amesema Mziray.
Amesema katika kipindi cha miaka mitano ya serikali ya awamu ya Tano Shehena/Mizigo 6,668 vya dawa ,Vifaa Tiba na Vitendanishi vilikaguliwa katika vituo vya forodha 10 ambavyo ni Sirari,Mtukula,Rusumo,Mulongo, Kabanga, Bandari ya Kusini Mwanza, Uwanja wa Ndege wa Mwanza,Bandari ya Ziwa Musoma, Bandari Kavu ya Isaka na Bandari ya Kamondo Bay na mizigo ambayo haiikukidhi vigezo vya ubora na usalama ilizuiliwa na baadae kuteketezwa na zingine bidhaa zilirudishwa katika nchi zinakotoka.
*Yapiga hatua katika uanzishaji wa viwanda vya dawa,vifaa tiba Kanda ya Ziwa.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii ,Mwanza
Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Ziwa katika kipindi cha miaka minne ya serikali ya awamu ya tano ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli imesajili na kutoa vibali vya majengo ya biashara ya Dawa, Vifaa Tiba na Vitandanishi 2,043.
Usajili na utoaji wa vibali ilitokana na TMDA Kanda ya ziwa baada ya kufanya ukaguzi na kujiridhisha kuwa majengo yankidhi vigezo vya utunzaji wa ,usambazaji ,uuzaji na utengenezaji wa bidha hizo.
Akizungumza na waandishi wa habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto , Meneja wa Kanda ya Ziwa Sophia Mziray amesema kuwa katika Miaka minne ya Utawala wa Rais Dkt.John Pombe Magufuli wamefanikiwa kutokana na serikali kuwekeza maabara ya uchunguzi wa dawa,Vifaa Tiba na Vitendanishi kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa za afya zilizo bora.
Amesema kuwa TMDA kwa kanda Ziwa imetoa ushauri wa kitaalamu katika kiwanda cha dawa kimoja cha jijini Mwanza pamoja na ushauri wa wa kiufundi kwa kwa viwanda saba vipya vya tiba na viwanda vinne vya vipya vya dawa za maji na sindano.
Mziray amesesma TMDA imeweka wakaguzi katika mipaka vituo vya forodha vya Sirari, Mtukula na Bandari ya Mwanza Kusini ambao ndio wakaguzi wa dawa,vifaa tiba na vitendanishi kuruhusu kuingia au kutoka nje ya nchi mara tu baada ya kujiridhisha katika ukaguzi.
Aidha amesema kuwa wameanzisha mfumo wa Kieletroniki wa uombaji wa vibali na utoaji kwa masaa 24 ambapo kupitia mfumo huu mkaguzi aliyeko mpakani ay bandarini anaweza kuhakikisha kibali kilichotolewa na mamlaka wakati wa kufanya ukaguzi wa bidhaa inayoingia kutoka nje ya nchi hadi sasa jumla ya vibali 2552 vimetolewa.
“Kwa kazi inayofanyika inaonyesha kuwa elimu ya udhibiti kwa wadau wetu imeeleweka na hivyo kukidhi matakwa ya kisheria ya uingizaji na utoaji wa bidhaa nje ya nchi”amesema Mziray.
Amesema katika kipindi cha miaka mitano ya serikali ya awamu ya Tano Shehena/Mizigo 6,668 vya dawa ,Vifaa Tiba na Vitendanishi vilikaguliwa katika vituo vya forodha 10 ambavyo ni Sirari,Mtukula,Rusumo,Mulongo, Kabanga, Bandari ya Kusini Mwanza, Uwanja wa Ndege wa Mwanza,Bandari ya Ziwa Musoma, Bandari Kavu ya Isaka na Bandari ya Kamondo Bay na mizigo ambayo haiikukidhi vigezo vya ubora na usalama ilizuiliwa na baadae kuteketezwa na zingine bidhaa zilirudishwa katika nchi zinakotoka.
Afisa Mwandamizi wa Ukaguzi wa Kanda ya Ziwa wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Bugaru Nyamweru akionesha maabara za uchunguzi ambazo serikali imewekeza kwa shi.bilioni Saba wakati wanadishi na maafisa habari wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo Jamii, Jinsia Wazee na Watoto walipotembele TMDA Kanda ya Ziwa,
Meneja wa Kanda ya Ziwa wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Sophia Mziray akizungumza na waandishi habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto , Meneja wa Kanda ya Ziwa Sophia Mziray amesema kuwa katika Miaka minne ya Utawala wa Rais Dkt.John Pombe Magufuli wamefanikiwa kutokana na serikali kuwekeza maabara ya uchunguzi wa dawa,Vifaa Tiba na Vitendanishi katika kanda hiyo.
Picha
ya Meneja wa Kanda ya Ziwa wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)
Sophia Mziray pamoja Waandishi Habari , Timu ya Maafisa wa Habari wa
Taasisi 17 zilizo chini ya Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,
Jinsia,Wazee na Watoto walipotembelea TMDA Kanda ya Ziwa.





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...