Sehemu ya waandishi wa habari za mazingira kutoka vyombo mbalimbali nchini wakiwa kwenye mafunzo yaliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira(JET) hivi karibuni jijini Dar  es Salaam kwa lengo la kuwajengea uwezo.

Mkurugenzi Mtendaji wa JET John Chikomo(kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya JET Dk.Ellen Utaru  Okoedion wakijadilana jambo wakati wa mafunzo hayo.



:Mwandishi Sidi Mgumia akitoa uzoefu wake katika masuala ya uandishi wa habari za mazingira na uhifadhi wakati wa semina hiyo iliyoandaliwa na JET hivi karibuni jijini Dar es Salaam.


:Baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari wakiwa katika semina ya waandishi wa habari za mazingira iliyofanyika hivi karibuni.


Mhariri mkongwe Jackton Manyerere(kulia) na Mwandishi Mwandamizi wa gazeti la Nipashe Salome Kitomari(kushoto)wakifuatilia kwa mafunzo yaliyohusu namna ya kuandika habari za mazingira na uhifadhi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya JET Ellen Utaru Okoedion (aliyesimama) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari za mazingira


Na Said Mwishehe, Michuzi Globu ya jamii

 CHAMA cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania(JET) moja uya mkakati wake ni kuhakikisha inaendelea kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini kuwa na uelewa mpana wa kuandika habari za mazingira na uhifadhi.

JET wamekuwa na utamaduni wa kuandaa mafunzo kwa waandishi wa habari na hasa waliojikita kwenye kuandika habari zinazohusu mazingira nchini. Kwa sehemu kubwa mafunzo hayo yamekuwa chachu kubwa ya kuifanya jamii nayo kupata habari sahihi zinazohusu mazingira kupitia waandishi ambao wamepita kwenye mikono ya JET.

Kwa kutumia watalaamu wa masuala ya mazigira na uhifadhi kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania wamekuwa daraja na kiunganishi muhimu katika ya wadau wa mazingira wakiwemo waandishi wa habari.

Mbali ya JET kutoa mafunzo yanayohusu mazingira na uhifadhi imekuwa na uratibu wa kuandaa ziara katika maeneo mbalimbali ya uhifadhi nchini na hivyo kutoa fursa kwa waandishi kujifunza kwa vitendo.

JET wamekuwa wakifanikisha mafunzo na ziara hiyo kupitia ushirikiano uliopo kati yao na  na USAID-Protect ambao wamekuwa wadau wakubwa na wa muda mrefu katika kuhakikusha mazingira na uhifadhi nchini Tanzania unakuwa salama.

Kwa kukumbusha tu JET imekuwa na mtandao mpana wa waandishi wa habari ambao ni sehemu ya wanachama wao na kwa sehemu kubwa wamejikita kuandika habari zinazohusu mazingira .

Hivyo kwa JET kwa kutambua umuhimu wa uhifadhi wa mazingira nayo imeamua kubeba jukumu la kuhakikisha inatumia kila aina ya chombo cha habari kuhakikisha umma wa Watanzania unakuwa na taarifa sahihi zinazohusu eeo hilo. Hakika JET wamefanikiwa na wanastahili pongezi kutokana na kubeba jukumu hilo kwa maendeleo ya Taifa letu.

Katika muendelezo huo wa utoaji wa mafunzo, siku za hivi karibuni JET iliandaa mafunzo maalumu kwa waandishi wa habari za mazingira ambapo mada mbalimbali zilitolewa kupitia watalaamu waliobobea kwenye sekta ya mazingira na uhifadhi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika hivi karibuni  jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa JET, Dk. Ellen Otaru ametumia nafasi hiyo kufafanua Chama hicho kimejitahidi kuboresha ufikishwaji wa taarifa kwa mwananchi ili mtanzania aelewe kuhusu mazingira anayoishi na jinsi ya kuishi nayo bila kuleta uharibifu.
 

"Yote tunayoyafanya tunamuelisha Mtanzania kwa ujumla wake ili afahamu kwa kina nini maana ya mazingira, nafasi yake kwenye hayo mazingira na yale mazingira yana umuhimu gani kwa faida yake na nchi yetu kwa ujumla,"amesema na kuongeza ili kuifikisha elimu hiyo kwa usahihi lazima wanayoipeleka nao wawe wameelimishwa vya kutosha

Dk.Otaru amesema  JET imekuwa mdau mkubwa katika   kupanga mikakati ya sera na sheria katika kuangalia inafanya vipi kuhakikisha inafanikiwa na kama zinakwenda sambamba na mahitaji yote hayo yanatokana na kalamu za wanahabari na nini kikifanyika jamii itaweza kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa mazingira.


Hata hivyo amesema JET inafanya yote hayo kama sehemu ya lengo la kundeleza kizazi hadi kizazi ili kiweze kupata yale ambayo wao wameyarithi kutoka vizazi vilivyopita na kwa kufanya hivyo kutasaidia jamii kuwa na uelewa na hatimaye kuyatunza mazingira ili nayo yawatunze.



"Ni wajibu wa kila mmoja wetu kufukiria nini kifanyike ili tuendeleze nchi yetu kwa kuangalia mfumo mzima wa wanyamapori,  binadamu pamoja na uchumi ambao wengi tunategemea kupitia wanyamapori," amesema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Nukta Afrika, Nuzulack Dausen akizungumza wakati wa mafunzo hayo amewahimiza  waandishi wa habari kufanya habari za uchunguzi zinazohusu wanyamapori na mazingira kwa lengo la kuelemisha jamii na kulinda hifadhi zilizopo kwa manufaa ya vizazi vijavyo.
 
Pia amewashauri waandishi wa habari kutumia kifaa cha kielektriniki kisicho na rubani (Drone) kwa ajili ya kufanya habari za uchunguzi kwenye maeneo ya hifadhi na mbuga za hapa nchini ili kubaini majangili wanaoingia katika hifadhi hizo.
 
"Ili mwandishi aweze kufanya habari yake vizuri ni lazima atengeneze 'network' na wakati anatengeneza lazima ajue uhusiano na watoa taarifa wake ili aweze kufanya kazi yake kwa njia rahisi na kujua nani ni nani na anafanya nini,"amesema.
 
Pia, amesema pindi mwandishi wa habari anapokwenda kufanya mahojiano anatakiwa kuuliza maswali mengi ili kupata mambo mengi ikiwemo kujua ulewa wa watu ambao anawafanyia mahojiano na hiyo itamsaidia kufahamu vitu vingi kwa wakati mmoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...