Ujenzi wa barabara za
lami katika mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma waanza kwa kasi ili kuimarisha mawasiliano na
huduma kwa wananchi.
Akizungumza leo Machi
20, 2020 katika mahojiano maalum, Katibu wa Kikosi Kazi cha Taifa cha Kuratibu
Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma Bw. Meshack
Bandawe amesema kuwa ujenzi huo
unahusisha barabara zenye urefu wa kilomita 39 ndani ya mji huo.
“Serikali inaimarisha
miundombinu ndani ya mji wa Serikali ikiwemo ujenzi wa barabara za njia mbili zenye urefu wa kilomita 28 na
zenye njia 4 kilomita 11, ujenzi huu unaenda sambamba na kujengwa kwa
miundombinu mingine kama TEHAMA, Afya, Makazi na Sehemu za Biashara”,
Alisisitiza Bandawe
Akifafanua Bandawe amesema kuwa ujenzi wa miundombinu katika mji wa Serikali
unaenda sambamba kujengwa kwa majengo ya gorofa kwa ajili ya matumizi ya Ofisi
za Wizara 22.
Mji wa Serikali
ulizinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mwezi Machi 2019.
Katibu wa Kikosi
Kazi cha Taifa cha Kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma Bw. Meshack Bandawe akionesha kazi ya ujenzi wa barabara
za lami inavyoendelea
Eneo lililosafishwa
tayari kwa ujenzi wa barabara za lami katika mji wa Serikali Mtumba Jijini
Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...