Katibu Tawala Msaidizi - Utawala na Rasilimaliwatu, James G. Bwana (Mwenye Shati Jeupe la Kitenge), akimkabidhi, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, Chamatata B.A, Kompyuta Mpakato ya kisasa na 'Work Station' yake ili iwe mali ya Ofisi (RS Shinyanga), makabidhiano yaliyofanyika jana Machi 18, 2020 ofisini hapo. Kompyuta Mpakato hiyo itatumiwa na Sehemu ya Utawala na Rasilimaliwatu na Ofisi kwa ujumla. Bwana alikabidhiwa Kompyuta hiyo na Katibu Mkuu Utumishi, Dkt. Laurean Ndumbaro, baada ya kukabidhi Komputa na Printa za kisasa zenye thamani ya Tshs. 45,919,500/= alizokabidhiwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP). Wengine pichani ni Afisa Tawala Mkuu, Bi. Beatrice Matemu (kushoto) na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi, Gervas Lugodisha (kulia).
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...