Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amefuta safari yake ya Italia kufuatia hofu ya ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama corona. Baada ya China, Italia sasa ndio nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu walioambukizwa na kufariki kutokana na ugonjwa wa COVID-19.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, hadi kufikia Machi 14, watu 17,660 walikuwa wameambukizwa kirusi cha corona Italia huku wengine 1,268 wakiwa wamepoteza maisha.

Kwa mujibu wa ripoti katika gazeti la Daily Nation, Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya imeufahamisha Ubalozi wa Italia mjini Nairobi kuwa Rais Kenyatta amefuta safari yake ya Italia iliyotarajiwa kufanyika kuanzia Machi 10 hadi 14.
 
 Rais Kenyatta alikuwa amepangiwa kutembelea mji mkuu wa Italia, Roma kwa lengo la kukutana na viongozi wa nchi hiyo na kisha aelekee Vatican kwa ajili ya kukutana na kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...