Kesi za maambukizi ya ugonjwa wa corona au COVID-19 barani Afrika zimepita 800 hadi kufikkia Ijumaa huku nchi mbalimbali zikiiimarisha hatua za kukabiliana na ugonjwa huo unaoenea kwa kasi kote duniani.

Kwa mara ya kwanza, Chad, Niger na Cape Verde zimeripoti kesi za maambukizi ya kirusi cha corona. Huko mashariki mwa Afrika, idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa kirusi hicho ikiongezeka katika nchi za Tanzania, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kwa mujibu wa taarifa aghlabu ya wagonjwa wa COVID-19 barani Afrika wametokea Ulaya na Marekani, na ili kuzuia ueneaji wa janga hili, nchi mbalimbali barani humo zimesimamisha safari za ndege kutoka nchi zilizokumbwa zaidi na janga hilo haswa nchi za Ulaya.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...