Na Woinde Shizza, ARUMERU
Wajumbe wa baraza la madiwani Halmashauri ya Meru, wilayani Arumeru, wamekubaliana kuwa na agenda ya kutokomeza mimba za utotoni na utoro shuleni kudumu kwenye vikao vya Vijiji na Kata kwa kujikita kuelimisha jamii kuanzia ngazi ya familia. 
Wajumbe hao wameadhimia hilo, mara baada ya, madiwani wa Kata kadhaa kuwasilishwa taarifa zinazoonesha changamoto ya mimba za utotoni zinazowaka bili wanafunzi katika kata zao. 
Awali taarifa hizo zimethibitishwa na Idara ya Elimu Msingi na Sekondari kuthibitisha kuwa jumla wanafunzi 67 wamepata mimba  kwa mwaka 2017/2018. 
Afisa elimu Sekondari Mwl Emmy Mkuru alieleza kuwa kwa kipindi cha Mwezi Januari 2017 mpaka sasa jumla ya wanafunzi 57 waliripotiwa kupata mimba ambapo kati yao  wanafunzi 27 wamepata mimba kuan zia mwezi Januari mwaka huu 2018.
Mwl.Emmy  ametoa rai kwa wazazi kutekeleza jukumu la malezi kwa wanafunzi sambamba na kujenga mabweni ili kuwaepusha wanafunzi  hao wa kike  na vishawishi  wanavyokutana navyo kwa kutembea umbali mrefu kwenda shule .
Nae mwakilishi wa Afisa elimu Msingi Makius Ngazi alieleza kuwa  kwa kipindi cha Mwezi Januari Mwaka 2017 hadi Mwezi Octoba mwaka huu jumla ya wanafunzi 10 wa shule za Msingi wamepata mimba na kushindwa kuendelea na Masomo.
Mwanasheria wa Halmashauri hiyo,wakili Magdalena John alisema Serikali iliweka sheria ili kumlinda Mwanafunzi kutokukosa fursa ya masomo  ila changamoto kubwa katika kushughulika na  kesi za mimba kwa wanafunzi ni utoaji wa ushahidi hivyo ametoa rai kwa wazazi na jamii kutoa ushahidi kwa wakati.
Makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Nelson Mafie amesikitishwa  na wazazi kutokua mstari wa mbele kutoa taarifa za wanafunzi kupata mimba na kusubiri viongozi kuja kuzitafuta. "tumeona hivi karibuni Mkuu  wetu wa Wilaya Jerry Muro akipambana kutokomeza mimba kwa wanafunzi kwa kuwachukulia hatua wahusika , hivi wazazi na jamii tunakuwa tupo wapi ?' " Alihoji Mafie .
"Halmashauri imejipanga vipi kumaliza swala la mimba kwa wanafunzi ?"amehoji Diwani viti maalumu Kata ya Usa -River Meri Antony 
Akihitimisha mjadala huo mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Will Njau, ametoa rai kwa viongozi wa dini ,mila na siasa kutoa elimu huku muongozo wa baraza hilo agenda ya kutokomeza mimba za utotoni kwa wanafunzi na utoro kuwa ya kudumu katika vikao ngazi za vijiji na kata .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...