Waziri Mkuu, Kaasim Majaliwa
akizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Ummy Mwalimu (wa tatu kulia) wakati alipokagua hospitali ya
wilaya ya kibaha iliyopo eneo la Lulanzi ambayo imetengwa kwa ajili ya
kuwahuduma kwa wagonjwa wa Coroma, Machi 28, 2020. Kulia ni Mkuu wa
Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo na wa pili kushoto ni Mganga
Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Bakari.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akikagua wodi za hospitali ya wilaya ya Kibaha iliyopo eneo la
Lulanzi ambayo imetengwa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wa Corona
Mchi 28, 2020. Kushto ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist
Ndikilio. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Waziri Mkuu: Hospitali Wilaya Kibaha itatumika kulaza wagonjwa wa Corona
Na.WAMJW-Kibaha
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ametembelea Hospitali mpya ya Halmashauri ya Wilaya Kibaha ambayo itatumika kulaza watakaobainika kuwa na Virusi vya ugonjwa wa Corona (Covid19).
Mhe.Kassim Majaliwa amesema hospitali hiyo itatumika kulaza watu walioambukizwa ugonjwa huo na kwamba itatumika kwa muda na baada ya ugonjwa huo kwisha itaanza kutoa huduma nyingine za afya.
Waziri Mkuu aliwaeleza wananchi wa Wilaya ya Kibaha kuwa watu wenye maambukizi ya VIRUSI vya COVID 19 watalazwa katika hospitali hiyo kwa muda wa siku 14 na baada ya uchunguzi ikibainika hawana ugonjwa huo wataruhusiwa kurejea nyumbani.
Mhe. Kassim Majaliwa amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya Corona na amezikumbusha familia kuwa na utaratibu wa kunawa mikono mara kwa mara kwa kutumia maji tiririka na sabuni au kutumia vitakasa mikono (sanitizer).
Awali, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu alimweleza Waziri Mkuu kwamba hospitali hiyo ilipokea kiasi cha shilingi milioni 394 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa hospitali hiyo.
Waziri Mkuu: Hospitali Wilaya Kibaha itatumika kulaza wagonjwa wa Corona
Na.WAMJW-Kibaha
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ametembelea Hospitali mpya ya Halmashauri ya Wilaya Kibaha ambayo itatumika kulaza watakaobainika kuwa na Virusi vya ugonjwa wa Corona (Covid19).
Mhe.Kassim Majaliwa amesema hospitali hiyo itatumika kulaza watu walioambukizwa ugonjwa huo na kwamba itatumika kwa muda na baada ya ugonjwa huo kwisha itaanza kutoa huduma nyingine za afya.
Waziri Mkuu aliwaeleza wananchi wa Wilaya ya Kibaha kuwa watu wenye maambukizi ya VIRUSI vya COVID 19 watalazwa katika hospitali hiyo kwa muda wa siku 14 na baada ya uchunguzi ikibainika hawana ugonjwa huo wataruhusiwa kurejea nyumbani.
Mhe. Kassim Majaliwa amewataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya Corona na amezikumbusha familia kuwa na utaratibu wa kunawa mikono mara kwa mara kwa kutumia maji tiririka na sabuni au kutumia vitakasa mikono (sanitizer).
Awali, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu alimweleza Waziri Mkuu kwamba hospitali hiyo ilipokea kiasi cha shilingi milioni 394 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa hospitali hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...