NA YEREMIAS  NGERANGERA….NAMTUMBO.
Bodi ya afya katika Halmashuri ya wilaya ya  Namtumbo mkoani Ruvuma imeridhishwa na ujenzi wa majengo ya kutolea huduma za afya  katika Halmashauri hiyo.
Akiogea wakati wa majumuisho ya ziara ya kukagua ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya  mjumbe wa bodi ambaye pia ni diwani wa kata ya Magazini bwana Saidi Ligulu alisema bodi ya afya  ya wilaya imeridhishwa na ujenzi  wa vituo vya kutolea huduma za afya zilizokaguliwa na bodi hiyo.
Aidha bwana Ligulu alimpongeza kaimu mganga mkuu wa wilaya ya Namtumbo bwana Godwin  Lutta kwa kuwaandalia ziara  ya kukagua na kujionea  ujenzi  wa vituo vya kutolea huduma za afya katika halmashauri ya wilaya ya Namtumbo ili waweze  kuwa wajumbe wazuri  kwa wananchi wanaowawakilisha katika maswala ya afya.
Hata hivyo  bwana Ligulu alipongeza ushirikiano uliopo kati ya kamati za ujenzi ,wananchi  wanaotoa nguvu zao katika kuhakikisha ujenzi uafanyika pamoja na uongozi wa Halmashauri katika kuhakikisha ujenzi huo unakidhi vigezo vilivyowekwa  na wizara ya afya.
Naye Antony Mbawala mjumbe wa bodi hiyo kutoka katika kata ya Msindo  kwa upande wake  pamoja na kumpongeza kaimu mganga mkuu kwa kuwaandalia ziara kujionea ujenzi wa vituo vya afya alidai ziara hiyo imewafanya watambulike na wahudumu wa vituo vya kutolea huduma za afya na kuongeza kuwa kitendo hicho kitawarahisisishia wajumbe hao kuhoji mambo mbalimbali katika vituo vya kutolea huduma za afya bila wasiwasi wowote tofauti na mwanzo ambapo wahudumu hao walikuwa hawawatambui pale walipotaka kuhoji mambo katika vituo hivyo.
Wajumbe  katika ziara hiyo walikubali kutumia magari yao binafsi ili kuepuka msongamano katika gari moja la halmashauri ili kujikinga na maambukizi  ya ugonjwa hatari  wa Corona.
Ziara ya wajumbe  hao wa bodi ya afya ilikagua ujenzi wa majengo nane ya hospitali ya wilaya ya Namtumbo ,ujenzi wa Zahanati ya ukiwayuyu  pamoja na ujenzi wa majengo ya kituo cha afya cha Mtakanini katika kata ya Msindo na kuridhishwa na ujenzi wa vituo hivyo vya kutolea huduma za afya.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...