Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

WAKATI vizuizi vikipungua nchini China ikiwa ni sehemu ya kupambana na virusi vya Corona (Covid -19)  klabu moja ya mpira wa miguu nchini humo imeeleza nia yake ya kurudisha mambo katika hali ya kawaida.

Klabu ya Guangzhou Evergrande imetangaza kuanza kazi ya kujenga uwanja wa mpira utakaobeba watazamaji  100,000, na utakua uwanja mkubwa zaidi ulimwenguni.

Imeelezwa kuwa uwanja huo umejengwa katika umbo la ya aina ya lotus  utagharimu dola za kimarekani Bilioni 1.7 (Yuan Bilioni 12) na unategemewa kumalizika mwishoni mwa mwaka 2022.

Aidha imeelezwa kuwa kazi ilianza Alhamisi iliyopita, huku lengo la kujengwa kwa uwanja huo ikielezwa ni kuweka alama mpya ya kiwango cha juu duniani ambapo uwanja huo umelinganishwa na jumba la Opera la Sydney na Burj Khalifa huko Dubai, pamoja na ishara muhimu ya mpira wa miguu wa China unaenda ulimwenguni.

Timu ya Guangzhou Evergrande imekua ikicheza kwenye uwanja wa Tianhe wenye uwezo wa kubeba watazamaji 60,000 tangu 2011.

Kujenga uwanja wenye uwezo wa kubebe watazamaji 100,000 imeelezwa kuwa inaweza kuzidi uwezo wa siti 99,354 za kambi ya Barcelona Nou, ambapo kwa sasa ndio uwanja mkubwa wa soka ulimwenguni.

Vilevile imeelezwa kuwa ubunifu wa uwanja huo ni kazi kutoka kwa mbunifu kutoka wa Amerika Hasan Syed, kufuatia wazo la awali kutoka kwa mwenyekiti wa kikundi cha Evergrande Xu Jiayin huku kubuni umbo la ya maua ya lotus inatokana  hali ya Guangzhou kuwa jiji la Maua.

Uwanja huo unajumuisha vyumba maalumu 16 vya (VVIP) vyumba vya kibinafsi vya VIP (152) eneo la Shirikisho la Mpira Duniani  (FIFA,) eneo la wanariadha, eneo la vyombo vya habari, na chumba cha waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa ESPN, Xia aliwaambia waandishi wa habari kwamba Evergrande ina mpango wa kujenga kati ya viwanja vitatu hadi vitano vyenye uwezo wa kubeba watazamaji  80,000 hadi 100,000 ikiwa ni sehemu ya kuwa mwenyeji wa kombe la dunia kwa siku za baadaye. 

Guangzhou Evergrande ni moja ya timu zilizofanikiwa zaidi nchini China na katika bara la Asia.

Klabu hiyo imeshinda Ligi ya China Super mara nane, na pia Ligi mbili za Mabingwa barani Asia ikiwa ni  Klabu ya pekee ya China kushinda mara mbili.

Msimu wa soka (CS20) wa 2020 ulikuwa umepangwa kuanza mnamo Februari 22  uliahirishwa kwa sababu ya janga la coronavirus ambapo China ilikua nchi ya kwanza kuripoti janga hilo mwishoni mwaka jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...