Familia ya aliyekuwa mbunge wa Mafia marehemu Kanali mstaafu Ayoub Kimbau tumepokea msiba wa ndugu yetu kaka yetu jamaa yetu mbunge mstaafu wa Mafia Ndg. Abdulkarim IH Shah (Bujji) kwa mshtuko na masikitiko Makubwa sana...
Marehemu Shah (Bujji) pamoja na tofauti zetu za kisiasa baina yake na familia yetu hususan katika wakati wote wa zile kampeni za kisiasa, bado alikuwa ni mtu mwenye upendo nidhamu  utu heshima na uungwana wa hali ya juu hasa kwa wazazi wetu na sisi watoto.Buji alikuwa kaka, rafiki, mtani na kiongozi wetu mstaafu tutamkumbuka siku zote..
Mungu awatie nguvu na awape moyo wa subra ndugu na jamaa na watoto wake wote katika kipindi hiki kigumu...kipekee tunampa pole sana mke wa marehemu Bi. Naila kwa kumpoteza mwenza na baba wa watoto wake..
Mungu awape moyo wa subra na aweke roho ya marehemu kaka yangu rafiki yangu Bujji mahala pema peponi

ILWIR🙏
Omary Ayoub Kimbau
(Kwa niaba ya familia ya Kimbau)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...