Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

JIWE moja kubwa kati ya mawe makubwa yanayoelea nje ya uso wa dunia (asteroid)ambalo limepewa jina la 52768 (1998 OR2) linategemewa kupita pembeni ya dunia bila kuleta madhara yoyote hapo kesho Aprili 29, 2020, Shirika la utangazaji CNN limeripoti.

 Imeelezwa kuwa tukio hilo linatagemewa kutoka kesho katika majira ya 4:56 alfajiri  kwa mujibu wa Wakala wa vyombo vya anga za nchi za chini na anga za mbali nchini Marekani (NASA.)

Licha ya watu kuwa na sitofahamu kuhusiana na jiwe hilo na muelekeo wake wa kulenga dunia mtaalamu kutoka NASA Steven Pravdo amesema,  jiwe hilo litapita kilomita milioni 6 kutoka duniani na halitakuwa na athari yeyote.

Jiwe hilo linakadiriwa kuwa na ukubwa kati ya kilomita 1.8 hadi 4.1 litapita pembeni ya dunia kwa maili 3,908,792 ikitumia maili 29,461 kwa saa.

Imeelezwa kuwa jiwe hilo lililoanza kutua mwaka 1998 halitarajiwi kuleta athari yoyote.

Imeshauriwa wenye darubini za kuangalia anga za mbali wanaweza kuliona jiwe hilo likitembea anga za mbali taratibu mithili ya nyota katika tarehe tajwa.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...