Yassir Simba,Michuzi TV

Klabu ya Yanga imethibitisha kumalizana na kiungo wake mkabaji ambaye ni nahondha wa klabu hiyo raia wa Congo DRC Pappy Kabamba Tshishimbi ambaye mkataba wake ulikuwa unaelekea ukingoni mwishoni mwa msimu huu wa ligi kuu Tanzania bara.

Kiungo huyo ambaye siku za karibuni alikuwa akitajwa kuwaniwa na baadhi ya vilabu vya ligi kuu ikiwemo wekundu wa msimbazi Simba, rasmi sasa atasalia kwa wananchi hao wa jangwani mpaka 2022 kutokana na taarifa za awali kuwa ameingia kandarasi ya miaka 2 na mabingwa hao wa kihistoria.

Kupitia Mkurugenzi wa uwekezaji wa kampuni ya GSM Hersi Said amesisitiza kuwa, "Tshishimbi ni mali ya Yanga kwa sasa na haendi popote labda wanaomuhutaji wasubiri mpaka mkataba huu wa sasa utakapo malizika."
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...