Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MITANDAO mingi  ya kijamii ikiwemo Facebook, WhatsApp na TikTok, inaongelea video zao... video za  kundi linalofanya shughuli za mazishi kutoka nchini Ghana linalojulikana kama Prampram Pallbearers  ambalo kwa sasa limekua maarufu zaidi ulimwenguni kote.

Video la kundi hilo zinawaonesha wanaume watano waliovalia nguo nyeusi, miwani nyeusi wakiwa wamebeba jeneza wakisindikizwa na kibao cha "Astronomia" wimbo ulioimbwa na Tony Igy.

 Mwanzilishi wa kundi hilo Benjamin Aidoo akizungumza na "The Ghana report" ameeleza kuwa, alianza biashara hiyo mwaka 2007 na umaarufu wao mpya unaweza kushawishi kupandisha viwango vya huduma mara baada ya janga la Corona (Covid -19) kumalizika.

"Umaarufu ambao tunaupata sasa unakuza biashara yetu na tunaweza kuongeza gharama baada ya kutoweka kwa mlipuko wa virusi vya Corona na kwa sasa tuna msimamizi na wakili nchini Kenya" ameeleza. 

Aidoo amesema kuwa lazima kuwa mbunifu zaidi ili kufanikisha jambo lako;

" Hapa Ghana lazima uwe mbunifu, niligundua kuwa katika mazishi watu wengi huvaa nguo nyeusi lakini nilitaka kwangu iwe tofauti kwa hiyo nikaongeza rangi nyeupe, nyeusi na nyekundu" amesema.

Akifafanua kiwango cha gharama za huduma zao  Aidoo amesema, bei hutegemea na  mavazi waliyovaa na kusema kuwa mavazi meusi na meupe kwa kikundi hicho katika shughuli za mazishi ni gharama za chini zaidi kwa kampuni hiyo.

Kuhusiana na gharama za huduma hiyo Aidoo amesema kuwa kiwango cha juu zaidi ni dola za kimarekani 3000 ukiondoa usafiri, chakula na malazi kwa shughuli waliyoifanya nje ya nchi.

Pia ameeleza kuwa kundi hilo la mazishi litaendelea kuongeza vionjo ili kuweza kuendelea kuwa tofauti.

Akieleza uzoefu wa kazi hiyo, Aidoo amesema kuwa;

 "Tulifanya kazi kwa familia moja huko Kumasi mwaka jana, maiti ilikuwa nzito kiasi kwamba hatukuweza kunyanyua kidole kwa wiki mbili baada ya hapo" amesema Aidoo.

Kwa sasa ambapo dunia inapambana na mlipuko wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona mabango makubwa yenye picha ya wanaume hao yanaongezeka kote ulimwenguni ikiwa ni ishara ya  kuwahimiza watu kukaa nyumbani au kujiunga nao kama maiti kwenye sinema yao ya kurudi kwenye kaburini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...