Idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona (Covid-19) nchini Kenya imefikia 110 baada ya watu wengine 29 kuthibitishwa kuwa navyo ndani ya saa 24 zilizopita.
Akizungumza katika mkutano na wanahabari jijini Nairobi waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema kwamba watu wengine wawili wamepoteza maisha yao kutokana na maambukizi ya virusi hivyo.
Amesema kwamba idadi hiyo inaongeza idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo kufikia watatu. Kagwe ameongezea kwamba wagonjwa waliofariki wanatoka miji ya Nairobi na Mombasa.
Akizungumza katika mkutano na wanahabari jijini Nairobi waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema kwamba watu wengine wawili wamepoteza maisha yao kutokana na maambukizi ya virusi hivyo.
Amesema kwamba idadi hiyo inaongeza idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo kufikia watatu. Kagwe ameongezea kwamba wagonjwa waliofariki wanatoka miji ya Nairobi na Mombasa.
Waziri huyo pia amepiga marufuku usafiri wa Wakenya kuelekea katika
maeneo ya mashambani akionya kwamba huenda wakapeleka maambukizi ya
virusi hivyo katika maeneo hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...