Idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona (Covid-19) nchini Kenya imefikia 110 baada ya watu wengine 29 kuthibitishwa kuwa navyo ndani ya saa 24 zilizopita.

Akizungumza katika mkutano na wanahabari jijini Nairobi waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema kwamba watu wengine wawili wamepoteza maisha yao kutokana na maambukizi ya virusi hivyo.

Amesema kwamba idadi hiyo inaongeza idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo kufikia watatu. Kagwe ameongezea kwamba wagonjwa waliofariki wanatoka miji ya Nairobi na Mombasa.
 
Waziri huyo pia amepiga marufuku usafiri wa Wakenya kuelekea katika maeneo ya mashambani akionya kwamba huenda wakapeleka maambukizi ya virusi hivyo katika maeneo hayo.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...