Dkt. Grarvin Kweka wa Hospitali  ya Taifa ya Muhimbili akionesha namna ya kutumia vitakasa mikono kwa wafanyakazi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (Covid 19) wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na kufanyika katika ofisi za Bodi hiyo Jijini Dar es Salaam.
Dkt. Grarvin Kweka wa Hospitali  ya Taifa ya Muhimbili akitoa mada ya namna ya kujikinga na virusi vya Corona kwa  wafanyakazi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (Covid 19) wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na kufanyika katika ofisi za Bodi hiyo Jijini Dar es Salaam.
 
 
 Wafanyakazi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) wakifuatilia kwa umakini mafunzo yaliyotolewa na madaktari juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (Covid 19)  na virusi vya Ukimwi. Mafunzo yaliandaliwa na kufanyika katika ofisi za Bodi hiyo Jijini Dar es Salaa
 
 
 
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Wafanyakazi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) wamepatiwa mafunzo ya jinsi ya kujikinga na maambukizi ya  virusi vya CORONA ili kumpa fursa mtumishi kujua hali yake na hivyo kuchukua hatua zaidi za kujilinda na kuwalinda wengine.

Mafunzo hayo yameendana sambamba na upimaji kwa hiari wa HIV, Homa ya Ini, Shinikizo la Damu, kisukari Kisukari na ulinganifu wa urefu na uzito yaliyofanyika kwa siku moja ndani ya Ofisi za TTB Jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo  yalianza kwa  maombi maalum ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono kauli ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya kutumia siku tatu kuliombea Taifa liepushwe na janga la ugonjwa  wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya COVID 19.

Wafanyakazi wa TTB, waliweza kupata elimu hiyo muhimu pamoja na namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo ili kufanya kazi kwa ufanisi na kuongeza tija kwa shirika na taifa kwa ujumla.    

Katika mafunzo hayo, mada zilitolewa na Wataalam wa Afya  kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili  Dkt. Garvin Kweka kwa kushirikiana na Dkt. Hafidh Ameir wa Tanzania CommisionCommission for AIDS (TACAIDS). 

Kwa pamoja madokta hao, walitoa elimu inayowataka wafanyakazi hao kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona ambapo Shirika la Afya la Dunia (WHO) limetangaza kama janga la dunia na takribani watu milion  2,416,135 wamepata maambukizi, waliopona ni 632,983 na vifo ni 165,939 kwa dunia nzima.

 Wafanyakazi wa TTB Wametakiwa kujikinga na kuwakinga wengine wakiwa wanatoa huduma kwa jamii pamoja na jamii inayowazunguka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...