WAUMINI wa Dini ya Kiislam wakiwa katika Ibada ya kuusalia Mwili wa Marehemu Marin Hassan Marin, Mwandishi wa Habari Muandamiziu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) sala na dua hiyo imefanyika katiuka Msikiti wa KMKM Kibweni Wilaya ya Magharibi”A” Unguja leo 2/4./2020,saa nne na kuzikwa katika Makaburi ya Mwanakwerekwe Jijini Zanzibar.
WAUMINI wa Dini ya Kiislam wakiuombea dua mwili wa Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa Shirika la Habari Tanzania (TBC) baada ya kumalizika Sala ya Maiti iliofanyika katika Msikiti wa KMKM Kibweni Jijini Zanzibar
MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Ayoub Rioba akizungumza na kutowa shukrani baada ya maziko ya Mfanyakazi wake Mwadishi Muandamizi Marehemu Marin Hassan Marin, yaliofanyika katika makaburi ya mwanakwerekwe Jijini Zanzibar.
WAZIRI wa Habaro Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar.Mhe. Mahmoud Thabot Kombo akizungumza na kutowa shukrani kwa niaba ya Wizara yake wakati wa hafla ya maziko ya Mwandishi wa Habari Muandamizi Tanzania Marehemu Marin Hassan Marin, yaliofanyika katika makaburi ya Mwanakwerekwe Jijini Zanzibar
MWAKILISHI wa Familia ya Marehemu akitowa neno la shukrani kwa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa ushirikiano wao katika kufanika msiba huo.
MAWAZIRI wa Habari wa SMT na SMZ. Kushoto Waziri Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe. Mahmoud Thabit Kombo na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe, wakiwasili katika viwanja vya Msikiti wa Kibweni KMKM kuhudhuria maziko ya Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Marin Hassan Marin, yaliofanyika leo 2/4/2020 na kuzikwa katika makaburi ya Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.
WANANCHI wakibeba Jeneza lililokuwa na Mwili wa Marehemu Marin Hassan Marin, wakitoka  nyumbani kwa marehemu na kuelekea katika Msikiti wa Kibweni KMKM kwa ajili ya kuombea dua kwa ajili ya maziko yaliofanyika katika makaburi ya Mwanakwerekwe Jijini Zanzibar.
WAUMINI na Wananchi wakishiriki katika kisomo cha Hitma na Dua kumuombea Marehemu Marin Hassan Marin, iliofanyika nyumbani kwao Kibweni Wilaya ya Magharibi “B” Unguja wakati wa hafla hiyo ya maziko yaliofanyika leo 2/4/2020 saa nne asubuhi na kuzikwa katika makaburi ya Mwanakwerekwe Jijini Zanzibar.(Picha na Othman Maulid)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...