Na Leandra Gabriel, Michuzi Media TV

LEO Aprili 2 dunia inaadhimisha siku ya kimataifa ya kuhakikisha ukweli wa taarifa juu ya mambo yanayosikika ( World Fact Checking Day) ni siku ya kila mmoja kutafakari juu ya taarifa kuhusu taarifa anayopokea na kuipeleka kwa watu wengine.

Ikiwa ni maadhimisho ya tatu kufanyika mtandao wa uhakiki wa taarifa duniani (IFNC) umeeleza kuwa maadhimisho ya siku hiyo ni kwa kila mmoja wakiwemo wananchi, wanahabari na wataalamu wa uhakiki wa taarifa ikiwa ni katika kuzuia na kupambana na usambaaji wa taarifa zisizo na ukweli.

Katika maadhimisho hayo kwa mwaka huu wananchi kote duniani wameshauriwa kusambaza taarifa za kweli zilizothibitishwa na kutolewa na mamlaka husika katika wakati huu ambao dunia inapambana na janga la virusi vya Covid 19.

Imeelezwa kuwa ni wajibu wa kila mmoja kupunguza na kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo na hiyo ni pamoja na kufahamu vyanzo vya kuaminika vya taarifa ni hatua muhimu kabisa. 

Wataalamu kutoka mtandao wa uhakiki wa taarifa duniani (IFNC) wamewashauri wananchi kote duniani kutumia mitandao ya kijamii vyema kwa kutoa taarifa za kuelimisha zaidi jamii kuhusiana na mlipuko wa virusi vya Corona.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...