Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

BRAZIL ni nchi kubwa katika bara la Amerika ya Kusini, huku jina la nchi hiyo ikitokana na mti uliojulikana 'Brazilwood' kireno inaitwa Brasil ambayo ni lugha rasmi nchini humo, Brazil ni nchi pekee inayozungumza Kireno Amerika Kusini huku ikiwa na watu zaidi ya milioni 200 na imepakana na nchi zote za Amerika Kusini isipokuwa Chile na Ecuador.

 Brazil ilikuwa koloni ka wareno kwa miaka 322 kabla ya kupata uhuru wake 1822, na imekua nchi ya mwisho kabisa kukomesha biashara ya utumwa mwaka 1888 huko Amerika,  pia Brazil ni nchi ya tano kwa ukubwa duniani kijiografia na kwa idadi ya watu, Mji mkuu wa Brazil ni Brasilia na mji mkubwa zaidi ni Sao Paulo huku miji mikubwa ikiwa Rio de Janeiro, Salvador na Fortaleza.

Ikiwa moja ya nchi yenye uchumi mkubwa Brazil inafanya shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo hasa kahawa zao ambalo linazalishwa kwa wingi nchini humo tangu miaka 150 iliyopita, uchimbaji madini, uvuvi pamoja na shughuli za utalii ambapo kwa mwaka watalii zaidi ya milioni 6 hutembelea nchi hiyo lakini bado wanakumbana na matatizo kama umaskini, kutokuwa na usawa, changamoto za kiutawala na mazingira.

Brazil ina jumla ya viwanja vya ndege zaidi ya 700 katika miji 639, pamoja na hazina kubwa ya mto wa Amazon ambao ni wa pili kiukubwa duniani ukitanguliwa na mto Nile na hiyo ni pamoja na wanyama wa kipekee wakiwemo jaguars na pumas.

Brazil pia ipo vizuri katika sekta ya michezo, timu ya taifa ya mpira wa miguu nchini humo ni moja kati ya timu bora zaidi duniani na imetwaa kombe la dunia mara tano huku ikiwa na wachezaji maarufu kama Neymar, Ronaldo na Anderson Silva.

Tukio kubwa lililovunja rekodi kwa mujibu wa Guinness Book of World Records ni lile la Agosti 6-7, 2006 ambapo kikundi cha watu 10 kilivamia benki na kuiba fedha zipatazo dola za kimarekani 70 milioni katika mji wa Fortaleza. 

Pia katika mji wa Sao Paulo umetajwa kuwa eneo lenye foleni zaidi (Traffic jam) hasa nyakati za jioni, imewahi kurekodiwa kuwa na foleni kwa kilometa 309 kwa mwaka 2013.

Jardim Gramacho ni dampo kubwa duniani lililogundulika katika mji wa Duque de Caxias nchini humo na lilifungwa mwaka 2012.

Licha ya hayo Brazil ina upekee wa jumla ya vivutio 72 ikiwa inaongoza kwa kuwa na vivutio vingi katika bara la Amerika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...