Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
WENGI
 hufikiri kuwa kuzaliwa kawaida ni kawaida, ila kwa Claudio Viera de 
Oliveira ni tofauti kabisa, yeye amezaliwa kichwa kikiwa kimeangalia juu
 pamoja na ulemavu wa mikono na miguu,na alipozaliwa madaktari 
walimshauri mama yake Maria Jose Vieira amuache Claudio afe kwani 
angemsumbua mno katika malezi lakini mama yake alipuuzia ushauri huo.
Licha
 ya ulemavu huo Claudio hakukata tamaa, akiwa na miaka 40 aliweza 
kuandika kitabu kilichohusu maisha yake kiitwacho  'Omundo Esta Ao 
Contrario:
Claudio raia 
wa Brazil alizaliwa na tatizo hilo ambalo hutokea mara chache sana, 
kitaalamu linajulikama kama 'arthrogryposis' hali ya misuli katika 
sehemu ya mwili kushindwa kujikunja na kujikunjua na kubaki ikiwa 
imekakamaa.
Claudio
 alianza kujifunza kuandika kwa kutumia mdomo ili aweze kupambana na 
changamoto iliyokuwa ikimkabili na aliweza kutimiza ndoto yake ya kuwa 
mhasibu pamoja na kutoa mihadhara katika matukio mbalimbali.
Akiwa
 na miaka 40 alichapisha kitabu chake cha kwanza kiitwacho  'Omundo Esta
 Ao Contrario' ambacho kimeelezea maisha yake  na uzoefu alioupata 
kupitia hali yake pamoja na mchango wa mama yake katika kufikia malengo.
Mama
 wa kijana huyo amewahi kueleza vyombo vya habari kuwa alishauriwa na 
madaktari kumwacha kijana wake afariki dunia kwa kuwa asingeweza kupumua
 vizuri na wengine walimshauri asimpe chakula lakini hakusikiliza 
ushauri huo.
"Alianza 
kutembea mwenyewe baada ya kubebwa kila mahali kwa miaka nane na 
alijifunza kufanya vitu kama watu wengine bila kuhitaji msaada, mwanangu
 anajiamini sana ninajivunia" alieleza mama huyo.
Claudio
 amenukuliwa akieleza kuwa tangu alipokuwa mtoto hakupenda kuwategemea 
watu wengine daima alikuwa akijishughulisha na kazi na amekuwa 
akijifunza kupitia televisheni, simu, redio pamoja na mitandao 
mbalimbali hadi akatimiza ndoto na kutunukiwa shahada ya uhasibu katika 
chuo kikuu cha Feira de Santana.


 


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...