Na Woinde Shizza,Arusha

Uongozi wa bar maarufu ya picnic iliyopo katikati ya jiji la Arusha umeelezea mikakati mbalimbali ambayo wanaitekeleza kipindi hiki katika kupambana na janga la ugonjwa hatari wa  Corona.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa bar hiyo, Bodia Kaaya alisema kwamba kufuatia janga la corona wao kama watoa huduma wamechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuhakikisha wahudumu wao wanavaa barakoa muda wote wakati wa kutoa huduma.

Kaaya,alisema kwamba mbali na barakoa pia wamehakikisha wameweka ndoo za maji na sabuni katika milango ya kuingilia ndani ya eneo lao ili kunawa mikono yao kabla hawajaingia kupata huduma.

Alisema kwamba wametoa vitakasa mikono lakini pia wanapulizia dawa katika meza mbalimbali zilizopo ndani ya eneo lao kama njia mojawapo ya kupambana na corona.

Pia alisisitiza wanafuata kanuni zote zilizotolewa na wizara ya afya nchini ambapo wanawafundisha watumishi wao namna ya kuchukua tahadhari na ugonjwa wa corona.

"Tunachukua tahadhari zote tunazoelekezwa na wizara ya afya lakini pia tunawafundisha wafanyakazi wetu namna ya kujikinga na gonjwa hili"alisema meneja huyo

Naye mtumishi wa bar hiyo,Elisante Charles alisema kwamba wao kama watumishi wameelekezwa hatua zote za kuchukua kujikinga na gonjwa la corona kama kuvaa barakoa muda wote wawapo kazini.

Charles, alisema kwamba baadhi ya watumishi wa afya wamekuwa wakipita mara kwa Mara katika bar hiyo na kuwapa elimu mbalimbali na kufanya ukaguzi na kuiomba serikali kufanya hivyo kwenye maeneo mengine

"Witumishi wa idara ya Afya hapa Arusha wametupatia semina ya kutosha namna ya kujikinga na corona wakati wa kutoa huduma pia vifaa vipo vya kutosha uongozi umezingatia hilo na kufanya kazi kuwa rahisi alisema Charles.

Pichani ni Meneja wa Bar ya Picnic, Bodia Kaaya  akisafisha meza kwa kutumia dawa kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Corona (covid 19).
Picha meneja wa bar ya Picnic akimwagia mteja sabuni anawe mikono kabla ya kuingia Ndani ya bar hiyo kupata huduma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...